Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Gavana wa mkoa wa Darfur nchini Sudan ameshutumu jeshi kwa kushindwa kumaliza kuzingirwa kwa mji huo ambako kumekuwa kukiendelea kwa muda wa mwaka mmoja na kusababisha njaa kali katika mji wa El Fashir.
Minni Minawi, kiongozi wa zamani wa waasi, bado anaongoza idadi kubwa ya wapiganaji wa wanamgambo ambao wamesaidia jeshi kuzuia Vikosi vya Rapid Support Forces kuuteka mji huo.
Hali ya kibinadamu katika mji wa El Fashir inazidi kuwa mbaya siku hadi siku.
RSF wamekuwa wakijaribu kuuteka mji huo kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa.
Wamezuia misaada ya chakula isiingie, na kuwaacha raia wakiwa wamenaswa na kukabiliwa na njaa kali.
Sababu kuu kwa nini jeshi la Sudan limeweza kushikilia mji huo imekuwa msaada kutoka kwa wapiganaji chini ya usimamizi wa Minni Minawi.
Kiongozi wa zamani wa waasi sasa ameshutumu Jeshi kwa kutofanya vya kutosha kumaliza hali ya kuzingirwa.
Minawi alipendekeza uwezekano wa mazungumzo na RSF.
All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.