Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Utawala wa Trump umetangaza Jumanne kwamba utajiondoa tena kutoka kwa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sayansi na Utamaduni, UNESCO, hatua iliyotarajiwa ambayo inaonyesha Marekani ikijiondoa zaidi kutoka kwa mashirika ya kimataifa.
Uamuzi wa Marekani kusitisha ufadhili na kujiondoa UNESCO unakuja miaka miwili baada ya utawala wa Biden kujiunga tena kufuatia hali ya kutatanisha ya kujiondoa kwa kipindi cha miaka mitano kulikoanza wakati wa muhula wa kwanza wa Rais Donald Trump.
Ikulu ya White House ilitaja sababu zake kama ilivyokuwa mwaka 2018, ikisema inaamini kuhusika kwa Marekani sio kwa maslahi yake ya kitaifa na kushutumu shirika hilo kwa kuendeleza matamshi yanayopinga Israeli.
Uamuzi huo, ambao hautaanza kutekelezwa hadi Desemba 2026, utakuwa pigo kubwa kwa shirika hilo linalojulikana kwa kuhifadhi urithi wa kitamaduni kupitia mpango wake wa Maeneo ya Urithi wa Dunia wa UNESCO – ambao unatambua maeneo muhimu kwa ajili ya kutunzwa.
All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.