Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Rais wa Marekani Donald Trump ametangaza kuwa Marekani itapeleka “silaha za hali ya juu” nchini Ukraine kupitia nchi za Nato, huku pia akitishia kuitoza ushuru Urusi ushuru mkubwa ikiwa makubaliano ya kumaliza vita hayatafikiwa ndani ya siku 50.
“Tunataka kuhakikisha Ukraine inaweza kufanya kile inachotaka kufanya,” Trump alisema kufuatia mkutano na mkuu wa Nato Mark Rutte mjini Washington.
Rutte alithibitisha kuwa Marekani imeamua “kuipatia Ukraine kwa wingi kile ambacho ni muhimu kupitia Nato” na kwamba Ulaya itazingatia muswada huo.
Nchi za Ulaya zitaitumia Kyiv mifumo yao ya ulinzi ya anga ya Patriot – ambayo Ukraine inaitegemea kuzuwia mashambulizi mabaya ya anga ya Urusi – na silaha zaidi zitatolewa na Marekani, Trump alisema.
Si Rutte wala Trump aliyefafanua zaidi kuhusu silaha zitakazotumwa Kyiv lakini Rutte alisema makubaliano hayo yalijumuisha “makombora na risasi”.
All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.