Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Waandamanaji katikati ya mji wa nairobi siku ya Jumatano tarehe 25 Juni
Idadi ya raia waliofariki kutokana na maandamano ya siku ya Jumatano nchini Kenya imefikia watu 16.
Kwa mujibu wa Shirika la haki za kibinadamu Amnesty International wengi wamejuriwa ambapo miongoni mwa waliopoteza maisha, chanzo cha vifo vyao vimetokana na majeraha ya ya risasi.
Mkurugenzi mkuu wa Amnesty International Irungu Houghton anasema kwamba idadi hiyo imethibitishwa na tume ya kitaifa ya haki za kibinadamu nchini Kenya.
Maelfu ya vijana katika maeneo mbalimbali ya Kenya waliandamana kuadhimisha mwaka mmoja tangu maandamano mengine ya kupingwa muswada wa fedha yaliyosababisha mauaji ya zaidi ya watu 60.
Maandamano hayo yalifanyika mwaka jana mwezi Juni 25, ambapo mbali na vifo hivyo yalisababisha mamia kujeruhiwa.
All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.