Aina 5 Muhimu Za Nidhamu Binafsi Unazotakiwa Kuwa Nazo…

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

i. Nidhamu ya kihisia

ii. Nidhamu ya kifedha

iii. Nidhamu ya kujiendeleza

iv. Nidhamu ya kuhusiana na watu

v. Nidhamu ya muda

Katika Makala Hii Tutazungumzia Aina ya Kwanza ya Nidhamu Binafsi

– Nidhamu ya Kihisia

Kama hauwezi kujinidhamisha kuhusiana na hisia zako basi utapoteza hatima yako.

Kuna watu wengi wangeweza kuwa wakubwa ila wameshindwa kudhibiti hisia zao katika mapenzi, kula n.k kwa sababu hiyo wameharibu hatima zao.

Sio kila ambacho hisia zako zinakitamani basi unatakiwa kukipata, vingine unatakiwa kujizuia.

Moja ya kanuni kubwa na muhimu kwenye maisha ni ile inayoitwa “The Principle of Delayed Gratification”.

Kanuni hii inakutaka kujizuia mambo yanayokupa raha kwa muda mfupi ili ujijenge kwa ajili ya mambo yatakayokupa faida kwa mudamrefu.

Watu ambao wameshindwa kudhibiti hisia zao, wamejikuta wakiingia katika kufurahia mambo wakiwa chuoni ila yamewaletea madhara baada ya kutoka chuo.

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment