Bibi harusi apigwa risasi na kuuawa katika tafrija ya harusi yake Ufaransa

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Bibi harusi aliuawa kwa kupigwa risasi usiku wa kuamkia harusi yake katika kijiji karibu na mji wa kusini-mashariki wa Ufaransa wa Avignon baada ya watu waliokuwa wamejifunika nyuso zao kufyatua risasi, maafisa wa eneo walisema.

Mshukiwa mmoja wa shambulizi pia aliuawa katika tukio la kurushiana risasi, na bwana harusi na mtoto wa miaka 13 walijeruhiwa vibaya wakati wa kisa hicho katika kijiji cha Goult.

Msako unaojumuisha makumi ya maafisa wa polisi na helikopta unaendelea kuwatafuta washukiwa wasiojulikana ambao walifanikiwa kukimbia.

Vyombo vya habari vya Ufaransa vinaripoti kwamba ghasia hizo zinaweza kuhusishwa na mgogoro wa dawa za kulevya.

Mamlaka imefungua uchunguzi kuhusu mauaji na jaribio la mauaji.

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment