Rais Samia amteua Jaji Mkuu mpya Tanzania

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Rais Samia

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amemteua jaji wa Mahakama ya Rufani, George Mcheche Masaju kuwa jaji Mkuu wa Tanzania.

Jaji Masaju anachukua nafasi ya Profesa Ibrahim Hamis Juma ambaye amestaafu.

Januari mwaka 2015 aliteuliwa na aliyekuwa Rais wa taifa hilo, Jakaya Kikwete kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali baada ya AG Werema Kujiuzulu.

Novemba 2015 aliteuliwa tena na Rais wa wakati huo, John Magufuli Kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Februari 2018 aliteuliwa na Rais Magufuli Kuwa Jaji wa Mahakama Kuu.

Aprili 2023 Aliteuliwa na Rais Samia kuwa Mshauri wa Rais, Masuala ya Sheria.

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment