Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Zaidi ya wafungwa 200 wa kivita wa Ukraine wamekufa wakiwa kizuizini tangu kuanza kwa uvamizi nchini Ukraine, kulingana na ripoti ya Associated Press.
Likiwanukuu wanaharakati wa haki za binadamu, Umoja wa Mataifa, mamlaka za Ukraine na mtaalamu wa uchunguzi wa kimahakama, chapisho hilo linabainisha kuwa kutendewa kikatili katika magereza ya Urusi kunawezekana kuwa sababu ya vifo vingi.
Mamlaka ya Urusi haikuwa tayari kusema chochote kuhusu hilo.
Hapo awali waliishutumu Ukraine kwa kuwatendea vibaya wafungwa wa kivita wa Urusi, mashtaka ambayo Umoja wa Mataifa uliyaunga mkono kwa kiasi, lakini kwa tahadhari kwamba dhuluma za Ukraine hazijaenea sana na mbaya zaidi kuliko zile ambazo Urusi inashutumiwa.
Ripoti ya Umoja wa Mataifa ya 2024 ilisema 95% ya wafungwa wa Ukraine walioachiliwa waliteswa. Wafungwa walielezea vipigo, shoti za umeme, kukosa hewa, unyanyasaji wa kijinsia, kunyongwa kwa dhihaka na kukosa usingizi.
Ripoti hiyo pia ilisema kwamba baadhi ya wafungwa wa Urusi walinyanyaswa na vikosi vya Ukraine wakati wa kuwakamata mara ya kwanza, ikiwa ni pamoja na kupigwa, vitisho na shoti za umeme. Hata hivyo, unyanyasaji huo ulikoma mara tu wafungwa wa Urusi walipohamishiwa katika vituo rasmi vya kizuizini vya Ukraine, ripoti hiyo ilisema.
All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.