Bunge la Seneti DRC laondoa kinga ya kutoshtakiwa ya aliyekuwa rais wa nchi hiyo, Joseph Kabila

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Kabila

Bunge la Seneti la DRC limeondoa kinga ya aliyekuwa Rais wa nchi hiyo Joseph Kabila, na kumtengenezea njia ya kufunguliwa mashitaka.

Kabila ambaye pia ni seneta wa maisha, anatuhumiwa kwa uhaini, uhalifu wa kivita, na kuunga mkono kundi la waasi la M23 ambalo liliteka miji mikubwa Mashariki mwa Congo mapema mwaka huu.

Kwa jumla, Maseneta 88 walipiga kura ya kuunga mkono kushitakiwa kwake, ni watano pekee waliopiga kura dhidi yake, huku kura nyingine tatu zikibatilishwa. Joseph Kabila ambaye aliondoka nchini 2023 hakufika mbele ya seneti kujitetea kabla ya kura ya leo.

Anakuwa Mkuu wa kwanza wa zamani wa Nchi kushtakiwa kwa uhaini, uhalifu wa kivita na mashtaka yanayohusiana nayo.

All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment