Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amesema Sir Keir Starmer na viongozi wengine “wamesema wanataka Hamas ibaki madarakani”.
Pia aliwashutumu viongozi wa Uingereza, Ufaransa na Canada kwa kushirikiana na “wauaji wengi, wabakaji, wauaji wa watoto na watekaji nyara”.
Katika video iliyowekwa kwenye X , akizungumzia shambulio la Alhamisi dhidi ya wafanyakazi wa ubalozi wa Israel huko Washington DC, Netanyahu alisema Sir Keir, Emmanuel Macron na Mark Carney walitaka Israel “kukubali kwamba jeshi la Hamas la wauaji wa umati litanusurika”.
Downing Street imekataa kutoa maoni moja kwa moja juu ya matamshi ya Netanyahu, lakini ilionesha chapisho la Sir Keir la kulaani shambulio la Washington kwenye mtandao wa X.
All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.