Makosa 4 Wanayofanya Wanawake Wenye Uwezo Mkubwa Wanapokuwa Ndani Ya Ndoa…

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

i. Umemnyang’anya Mwanaume Nafasi Yake Ya Uongozi Kwenye Maisha Yako.

ii. Kushindana Na Mwanaume.

iii. Kumpa Nafasi Mwanaume Mwingine Kuwa Na Sauti Kwenye Maisha Yako Kuliko Mwanaume Wako.

iv. Kupoteza Haiba Ya Kike.

Katika Makala Hii Tutazungumzia Kosa La Nne

– Kupoteza Haiba Ya Kike

Sikiliza na uelewe dada yangu:

Moja ya kitu cha muhimu sana kwa mwanaume anachohitaji kutoka kwa mwanamke ni…

…“Feminine nature”, ile haiba na tabia zinazokutofautisha wewe na yeye.

Yaani, hata kama anakuita “Jembe langu”, usije hata siku moja ukaanza kuishi kama…

…mwanaume na kuonesha “Masculine nature”, utakuwa unajitengenezea shida.

Umeshawahi kusikia msemo wa “Jike Dume?”

– Hii inaelezea aina ile ya mwanamke ambaye anajiweka na kuwa na tabia kama za mwanaume.

Hata siku moja, hakuna mwanaume ambaye anataka kuishi na…

…mwanamke mwenye sifa na tabia za kiume kama yeye, hayupo.

Kuna maeneo yafuatayo ya kuwa nayo makini zaidi katika hili.

Eneo la kwanza ni muonekano wako.

Usijisahau dadangu, hakikisha muonekano wako bado…

…unabakia kuwa wakike bila kujali umezaa watoto wangapi.

Vaa kwa kupendeza, tunza nywele zako vizuri na nukia vizuri…

…hakikisha ukiwa naye anajivunia kuwa yuko na mwanamke mrembo.

Hii humfanya mwanaume ajisikie wajibu wa kukulinda…

…kukutunza na kukusapoti kwa sababu anajua yuko na mwanamke.

Eneo la pili ni kuonesha hisia zako.

Inajulikana mwanamke ni kiumbe cha hisia na wanaume hupenda hilo.

Usiache kuonesha hisia zako za kuwa “fragile”.

Muombe akusaidie vitu vya kubeba, kufanya…

…(Sio hadi balbu unafunga mwenyewe, kabati mlango ukiharibika unachukua nyundo unagonga n.k).

All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment