Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Mahakama ya rufaa nchini Mauritania imetoa hukumu ya kifungo cha miaka 15 jela na faini ya dola milioni 3 kwa Rais wa zamani Mohamed Ould Abdel Aziz baada ya kukata rufaa dhidi ya kifungo cha miaka mitano.
Aziz alisaidia kuongoza mapinduzi mawili kabla ya kuhudumu kwa mihula miwili kama rais wa nchi hiyo ya kaskazini magharibi mwa Afrika na kuwa mshirika wa kukabiliana na ugaidi katika mataifa ya Magharibi.
Alihukumiwa mwaka wa 2023 baada ya kupatikana na hatia ya utakatishaji fedha na kujitajirisha. Kulingana na wachunguzi, alikusanya mali yenye thamani ya zaidi ya dola milioni 70 akiwa madarakani. Amekuwa kizuizini tangu kutolewa kwa uamuzi huo.
Kesi hiyo ilikuwa tukio la nadra ambapo kiongozi wa Kiafrika alishtakiwa kwa ufisadi. Mawakili wa Aziz wamesema kesi hiyo imechochewa kisiasa.
Uamuzi huo wa Jumatano uliwaondolea kesi maafisa sita wakuu kutoka kwa utawala wa rais huyo wa zamani, lakini ukamhukumu mkwe wa Aziz kifungo cha miaka miwili jela kwa kosa la ushawishi.
Mauritania ina utajiri mkubwa wa maliasili ikijumuisha madini ya chuma, shaba, zinki, fosfeti, dhahabu, mafuta na gesi asilia.
Lakini bado karibu 60% ya watu wanaishi katika umaskini, kulingana na Umoja wa Mataifa, wakifanya kazi kama wakulima au waajiriwa.
All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.