Watu 21 wamepoteza maisha katika ajali iliyotokea Mexico – afisa amesema

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

.

Takriban watu 21 wamefariki katika ajali ya barabarani katikati mwa Mexico, kulingana na afisa wa eneo hilo.

Ajali hiyo ya magari matatu ilitokea kwenye barabara kuu kati ya Cuacnopalan na Oaxaca katika jimbo la Puebla Jumatano asubuhi, alisema Samuel Aguilar Pala, afisa wa serikali ya mtaa.

Bw Pala alisema watu 18 walifariki katika eneo la tukio na wengine watatu walifariki baadaye hospitalini.

Wengine kadhaa walijeruhiwa na wanapokea matibabu, aliandika kwenye mtandao wa X.

Kulingana na vyombo vya habari vya eneo hilo, ajali hiyo ilihusisha lori, basi na gari dogo.

Gazeti la Mexico la La Jornada linaripoti kwamba ajali hiyo ilitokea wakati lori la saruji lilipojaribu kulipita gari dogo.

Lilipokuwa likivuka kuelekea upande wa pili, lori hilo liligonga basi na kisha kugongana na gari la usafiri uso kwa uso kabla ya kuangukia kwenye bonde lililokuwa chini na kuwaka moto, La Jornada alisema.

All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a Reply