Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Rais wa Urusi Vladimir Putin hatahudhuria mazungumzo ya amani kwa ajili ya vita huko Ukraine yatakayofanyika Istanbul Alhamisi, licha ya wito kutoka kwa Volodymyr Zelensky wa Ukraine.
Ujumbe wa Urusi badala yake utaongozwa na msaidizi wa rais Vladimir Medinsky, kulingana na taarifa ya Kremlin.
Zelensky hapo awali alisema kuwa atahudhuria mazungumzo hayo na kukutana ana kwa ana na Putin iwapo rais wa Urusi atakubali, na akasema atafanya kila awezalo kuhakikisha mkutano huo unafanyika.
Rais wa Marekani Donald Trump pia hatahudhuria, kwa mujibu wa ripoti za vyombo vya habari, licha ya awali kudokeza angehudhuria iwapo Putin angekuwepo.
All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.