Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Mateka wa Israel na Marekani Edan Alexander ameungana tena na familia yake nchini Israel baada ya kushikiliwa na Hamas huko Gaza kwa muda wa miezi 19.
Mvulana huyo mwenye umri wa miaka 21 alikuwa akitumikia jeshi la Israel kwenye mpaka wa Gaza alipotekwa na wanamgambo wa Hamas tarehe 7 Oktoba.
Siku ya Jumatatu, Israel ilisitisha operesheni zake za kijeshi huko Gaza kwa saa chache ili kuwezesha uhamisho huo.
Afisa wa ngazi ya juu wa Hamas aliiambia BBC kuwa kutolewa kwake kulikusudiwa kuonyesha ishara ya nia njema na kama sehemu ya juhudi za kufikia makubaliano mapya ya kusitisha mapigano kabla ya ziara ya Rais wa Marekani Donald Trump katika Mashariki ya Kati siku ya Jumanne.
Bw Alexander anadhaniwa kuwa raia wa mwisho wa Marekani anayeshikiliwa na Hamas ambaye bado alikuwa hai.
Katika taarifa, familia yake ilimshukuru rais wa Marekani lakini pia iliitaka serikali ya Israel na wapatanishi kuendeleza juhudi zaidi ili kuwakomboa mateka 58 waliosalia.
Bw Alexander ndiye mateka wa kwanza kuachiliwa na Hamas tangu Israel ianze tena mashambulizi yake ya kijeshi tarehe 18 Machi, baada ya kumalizika kwa muda wa miezi miwili wa kusitisha mapigano.
All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.