Gachagua: Nilikuwa nimemaliza kabisa pombe haramu Mlima Kenya lakini sasa imerudishwa

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

“Tukichukua serikali, tutahakikisha kuwa pombe hizo zenye sumu zinaondolewa sokoni,” alisisitiza.

Alizungumza baada ya watu watatu kulazwa hospitalini baada ya kunywa pombe inayoshukiwa kuchanganywa na kemikali hatari katika eneo la Kangai.

Watatu hao walilalamika kuumwa na tumbo na kizunguzungu baada ya kunywa pombe hiyo kwenye baa kijijini.

Walihamishwa kutoka kituo cha afya cha Njegas hadi hospitali ya rufaa ya Kerugoya kwa uchunguzi zaidi wa kiafya.

Mnamo Februari 5 mwaka jana, watu kumi na saba walifariki katika eneo hilo hilo huku wengine kadhaa wakipofuka baada ya kunywa pombe yenye sumu.

Tukio hilo lilishtua taifa zima huku Wakenya wakilaumu serikali kwa kulegea katika jukumu lake.

Bw Gachagua alishutumu serikali kwa kutowajali watu wa eneo la Mlima Kenya.

“Tutalinda na kuwasaidia watu wetu tukichukua mamlaka,” alisema.

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment