Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Mwanafunzi wa shule ya upili kutoka Wisconsin aliwaua wazazi wake kama sehemu ya njama kubwa ya kumuua Rais wa Marekani Donald Trump, FBI imesema.
Nikita Casap, 17, ameshtakiwa kwa mauaji ya mama yake, Tatiana Casap, 35, na baba yake wa kambo Donald Mayer, 51, ambao walipatikana wamekufa nyumbani kwao mnamo 28 Februari.
Hati mpya ya upekuzi ambayo haijafungwa pia inadai kuwa simu ya mshukiwa ilikuwa na nyenzo zinazohusiana na kikundi cha Nazi kiitwacho Order of Nine Angles na sifa kwa Adolf Hitler.
Wachunguzi pia waligundua maandishi ya chuki dhidi ya Wayahudi ambapo mshtakiwa alidaiwa kuelezea mipango yake ya kumuua Trump kama sehemu ya lengo pana la kupindua serikali, kulingana na hati ya mahakama.
Mshukiwa huyo anatuhumiwa kwa mauaji ya kukusudia ya daraja la kwanza na makosa mengine saba ya uhalifu, ikiwa ni pamoja na kuficha maiti na wizi.
Wazazi hao walipatikana wakiwa wamekufa wakati viongozi wa eneo hilo walipotembelea nyumba yao katika kijiji cha Waukesha, karibu na Milwaukee, baada ya mvulana huyo kukosa kuhudhuria shule kwa wiki mbili.
Bw Mayer alikufa kutokana na jeraha la risasi kichwani, huku Bi Casap akifariki kutokana na majeraha mengi ya risasi mnamo Februari 11, kulingana na malalamiko ya uhalifu kuhusu kijana huyo.
Siku hiyo hiyo miili yao ilipogunduliwa, mshtakiwa alikamatwa na polisi katika jimbo la Kansas alipokuwa akiendesha Volkswagen Atlas ya 2018 mali ya Bw Mayer, wachunguzi walisema.
Ndani ya gari hilo kulikuwa na bastola ya Bw Mayer’s Smith & Wesson .357, kadi nne za pesa za wanandoa hao, “vipande vingi” vya vito vya thamani, sefu ya bei ya juu na sarafu ya $14,000 (£10,700), nyingi zikiwa ndani ya Biblia, yalisema malalamiko ya uhalifu.
Katika maandishi yaliyopatikana na wachunguzi, mshukiwa alionyesha imani ya wazungu na kutaka mauaji ya Trump yaanze mapinduzi ya kisiasa, kulingana na hati ya upekuzi.
Madai ya mauaji ya watu wawili “yalionekana kuwa juhudi za kupata njia za kifedha na uhuru muhimu kutekeleza mpango wake,” wachunguzi waliandika.
Nyaraka za mahakama zinadai mshukiwa alikuwa akizungumza na watu nchini Urusi kuhusu mipango ya kuwaua wazazi wake.
Mamlaka ilisema kijana huyo alilipia ndege isiyo na rubani na vilipuzi kutumia katika shambulio – na alikuwa na mipango ya kutorokea Ukraine.
All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.