Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa
Mwanamuziki kutoka Mali Rokia Traoré amefikishwa tena katika mahakama ya Ubelgiji siku ya Jumatano, Januari 8, kwa kesi ya kushindwa kuwasilisha mtoto ambayo inamkabili baada ya kuwasilishwa nababa ya binti yake. Binti yao huyo alizaliwa mwaka wa 2015, anaishi Mali na baba yake, raia wa Ubelgiji anadai kuwa hajamwona kwa miaka mitano.

Kusikilizwa kwa kesi hii kwa mara ya kwanza ilikuwa Desemba 23, lakini mahakama haikutoa uamuzi juu ya uhalali wa kesi hiyo, kwa sababu Rokia Traoré alikuwa amebadilisha mawakili.
Mnamo Desemba 23, kesi ya msanii wa Mali nchini Ubelgiji ilifupishwa, na jaji akaruhusu kucheleweshwa kwa wiki mbili kwa wakili mpya ambaye Rokia Traoré alikuwa amempata. Bado alipata fursa ya kuzungumza mbele ya mahakama, anaripoti mwandishi wetu wa mjini Brussels, Pierre Benazet.
Wakati wa kusikilizwa kwa kesi hiyo mnamo Desemba 23, Rokia Traoré alibainisha kwamba “kamwe hakukataa baba” kuwasiliana na binti yao, lakini “aliogopa kumleta Ubelgiji na kwamba atazuiliwa hapa”. Binti ya msanii wa Mali na mwigizaji Jan Goossens “alikulia nchini Mali, ameishi huko maisha yake yote na yuko vizuri katika masuala ya elimu”, ndio lakini “hajui Ubelgiji”, amebainisha wakili wake mpya, Dimitri de Béco.
Sven Mary, wakili wa Jan Goossens, amebainisha kwamba mteja wake “anataka kumuona binti yake, kama baba. Yeye haombi kuzuiliwa kwa binti yake, lakini kuwa na haki ya kumuona wakati wa likizo” nchini Ubelgiji. Wakili huyo pia amekumbusha kwamba Rokia Traoré alikuwa tayari amekamatwa Machi 2020 huko Paris, kisha akasafiri kwa ndege na binti yake kwenda Mali licha ya marufuku ya kuondoka Ufaransa.
Alikamatwa nchini Italia mnamo mwezi Juni
Kitendo cha kutoshiriki katika mashauri ya awali kilisababisha mahakama za Ubelgiji kumhukumu Oktoba 2023 kifungo cha miaka miwili jela kwa “kukosa kutoa mtoto”, hukumu nzito iliyokusudiwa, kwa mujibu wa wakili wake wa awali, kumshurutisha kurudi kwa mahakama za Ubelgiji. Mwanamuziki huyo mwenye umri wa miaka 50 kisha alipinga hukumu hii, ili aweze kuhukumiwa tena, wakati huu mbele ya mahakama.
Kwa nadharia, mahakama lazima sasa iamue juu ya uhalali wa kesi, yaani hatia yake na suala la malezi ya mtoto. Suala kuu la Rokia Traoré ni kuachiliwa kwa masharti, jambo ambalo mahakama ilikataa wiki mbili zilizopita.
Rokia Traoré alikamatwa mnamo Juni 20 nchini Italia, chini ya hati ya kukamatwa ya Ulaya iliyotolewa na Ubelgiji. Baada ya kukaa katika gereza karibu na Roma, alihamishiwa jela huko Brussels mwishoni mwa mwezi Novemba.
All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.