Hamas waorodhesha majina ya mateka 34 wanaonuia kuwaachia huru

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Raia wa Israel

Afisa mwandamizi wa Hamas ameikabidhi BBC orodha ya mateka 34 ambao kundi la Wapalestina linadai kuwa lipo tayari kuwaachia huru katika awamu ya kwanza ya makubaliano ya kusitisha mapigano na Israel.

Haijulikani ni wangapi kati ya mateka hao bado wako hai.

Miongoni mwa walioorodheshwa ni wanawake 10 na wanaume wazee 11 wenye umri kati ya miaka 50 na 85, pamoja na watoto wadogo ambao Hamas ilisema awali waliuawa katika shambulio la angani la Israel.

Pia kuna baadhi ya mateka waliodaiwa kuwa ni wagonjwa, ambao pia wamo kwenye orodha hiyo.

Ripoti kutoka Gaza inayosimamiwa na Hamas zinasema kwamba mashambulizi ya angani ya Israel yaliua zaidi ya watu 100 huko mwishoni mwa juma.

Hata hivyo, ofisi ya Waziri Mkuu wa Israel ilikanusha taarifa kwamba Hamas imetoa orodha ya mateka kwa Israel.

Mazungumzo ya kusitisha mapigano yaliendelea Doha, Qatar, mwishoni mwa juma, lakini mazungumzo hayo hayajafikia mafanikio makubwa hadi sasa.

“Kufikia sasa, uvamizi unaendelea kuwa mgumu juu ya makubaliano ya masuala ya kusitisha mapigano na kujiondoa, na hakuna hatua iliyochukuliwa,” alisema afisa huyo wa Hamas akizungumza kwa sharti la kutotajwa jina.

Awali, Hamas ilichapisha video ya mateka wa Israeli mwenye umri wa miaka 19, Liri Albag, akihimiza serikali yake kufikia makubaliano. Alikamatwa pamoja na askari wanawake sita wa jeshi kwenye kambi ya Nahal Oz, kwenye mpaka wa Gaza, wakati wa shambulio la Hamas mnamo Oktoba 7, 2023.

Kampeni ya kijeshi ya Israel ya kukabiliana na kundi la Hamas imesababisha vifo vya watu wasiopungua 45,805 katika Gaza kufikia Jumamosi, kwa mujibu wa wizara ya afya inayosimamiwa na Hamas.

Chanzo hicho hicho kinadai kuwa mashambulizi ya angani ya Israel yaliua watu 88 Gaza Jumamosi na Jumapili, shirika la habari la Reuters liliripoti vyanzo vya afya vikisema kuwa watu 17 walikufa katika mashambulizi manne tofauti ya Israeli katika eneo hilo.

Jeshi la Israel limesema Jumapili kuwa ndege zake za kivita zilishambulia zaidi ya maeneo 100 ya “magaidi” katika Ukanda wa Gaza mwishoni mwa juma, na kuua maelfu ya wapiganaji wa Hamas.

All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment