Jeshi la Ukraine: Ndege zisizo na rubani 34 zadunguliwa angani juu ya Ukraine

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

g

Jeshi la Urusi limefanya mashambulizi Ukraine kwa kutumia ndege 81, ulinzi wa anga wa Ukraine ukadungua ndege zisizo na rubani 34, na ndege nyingine 47 zilipotea mashinani, Jeshi la anga la Ukraine limeripoti.

Mikoa iliyoshambuliwa ni Poltava, Sumy, Kharkov, Kiev, Chernigov, Cherkasy, Kirovograd, Dnepropetrovsk, Odessa na Nikolaev, imesema ripoti hiyo

Katika mikoa ya Chernihiv na Sumy, nyumba za watu binafsi ziliharibiwa kutokana na mashambulizi hayo

Ijumaa Jeshi la Ukraine lilitoa tahadhari ya uvamizi wa anga kote nchini Ukraine.

Jeshi la anga la Ukraine liliripoti mashambulizi ya ndege zisizo na rubani za Urusi na tisho la mashambulizi ya makombora.

All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment