Madagascar: Viongozi wa kidini wanatoa ujumbe mkali viongozi

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Kama kila mwaka, wakati wa sikukuu, viongozi wa kidini huhutubia waumini wao kupitia hotuba zinazovuka mfumo pekee wa ibada kushughulikia mambo ya kitaifa. Mwaka huu, makanisa mawili yenye ushawishi mkubwa nchini yametoa ujumbe mkali. Kanisa la kwanza linalaani unafiki wa viongozi tawala, huku wa kanisa la pili likishutumu – bila kutaja moja kwa moja – viongozi kung’ang’ania madarakani. Ujumbe ambao umeikasirisha sana serikali katika hali ya wasiwasi baada ya uchaguzi. 

Kanisa kuu la Andohalo huko Antananarivo. Kama kila mwaka, wakati wa sikukuu, viongozi wa kidini huhutubia waamini wao kupitia hotuba zinazopita zaidi ya mfumo pekee wa ibada.
Kanisa kuu la Andohalo huko Antananarivo. Kama kila mwaka, wakati wa sikukuu, viongozi wa kidini huhutubia waamini wao kupitia hotuba zinazopita zaidi ya mfumo pekee wa ibada. AFP – MAMYRAEL

Upinzani na mashirika ya kiraia wanahoji ukweli wa uchaguzi wa manispaa wa Desemba 11, 2024.

Ujumbe uliochapishwa mnamo Desemba 24 ulitosha kutikisa likizo ya kawaida ya sikukuu. “Krismasi isiwe kama ile ya Herode, ya (mtu aliyepofushwa), mwendawazimu madarakani (…) ambaye hutafuta kwa njia zote kuficha ukweli” amesema mkuu wa Kanisa la Kiprotestanti FJKM. Kulingana na sura ya mfalme wa Yudea katika karne ya 1 KK, Mchungaji Irako Ammi Andriamahazosoa anaomba viongozi wasianguke katika vitendo vyya kidhalimu inavyojulikana vya mfalme huyu.

“Mashambulizi ya kujificha”

Maneno yanayofananishwa na “mashambulizi ya kujificha” ya ofisi ya rais wa Jamhuri ya Madagascar. Alipohojiwa na RFI, Lova Ranoromaro, msemaji wake anabaini kwamba Kanisa lazima “liungane na sio kuchochea chuki”. Siku chache baadaye, mnamo Desemba 31, Kanisa Katoliki, likibembelezwa na Rais Andry Rajoelina, pia lilitoa ujumbe wa kutisha, ingawa kulikuwa na maeneo kidogo ya busara.

“Kupiga mayowe “Haleluya” na “Amina” kwa Kanisa hakuna maana ikiwa tutaendelea kufanya maovu,” anasema Kadinali Désiré Tsarahazana. Akitoa mfano wa kuendelea kwa vitendo vibaya ndani ya utawala. Wiki iliyopita, mbunge na maafisa watatu kutoka Wizara ya Mambo ya Nje walitiwa mbaroni katika visa viwili tofauti vya ulanguzi wa dhahabu na kasa.

Kanisa, mojawapo ya ngome za mwisho

Ujumbe wa viongozi wa kidini unaendelea kuwasilishwa na kutolewa maoni katika nyanja za umma na kisiasa. Kukiwa na upinzani dhaifu na chama cha rais chenye nguvu nyingi, Kanisa linachukuliwa kuwa mojawapo ya ngome za mwisho za wakazi nchini Madagascar, waliokwama katika maisha ya kila siku yalnayotokana na kupanda kwa gharama ya maisha pamoja na kukata kwa maji na umeme.

All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment