Khamenei anakosoa kuwepo kwa vituo vya Marekani katika ardhi ya Syria

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

h
Maelezo ya picha,Kiongozi Mkuu wa Iran Ali Khamenei

Katika siku ya kumbukumbu ya kuuawa kwa Jenerali Qassem Soleimani wa Iran, Kiongozi mkuu wa Iran Ayatollah Ali Khamenei alikosoa kile alichokitaja kuwa ni shambulio dhidi ya ardhi ya Syria, na kushambulia uwepo wa vituo vya Marekani nchini Syria.

Akizungumza Jumanne Khamenei alisema, “Syria ni ya Wasyria, na yeyote atakayeshambulia ardhi ya Syria bila shaka atalazimika kuondoka mbele ya upinzani wa vijana wa Syria.”

Ameongeza kuwa, “kambi za Marekani nchini Syria bila shaka zitaharibiwa na vijana wa Syria…”, kwa mujibu wa kile kilichoripotiwa na shirika la habari la Iran na vyombo vya habari vya Iran vilivyo karibu na Tehran.

Aliendelea kusema: “Iwapo nchi itaondoa vipengele vya uthabiti na nguvu zake kwenye medani, itakuwa kama Syria na itakuwa rahisi kukaliwa kama inavyotokea Syria, Marekani, jumuiya ya Kizayuni na baadhi ya nchi za kieneo .”

All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment