Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa
Olimpiki za Paris iliangaza majira ya joto kwa matukio ya kusisimua. Rekodi zilivunjwa, na mashujaa walijitokeza katika michezo tofauti kuanzia kwenye soka, riadha, ngumi, voliboli, basketiboli na michezo mingine mingi.

Tunapofunga mwaka 2024, ni wakati wa kutafakari matukio makubwa ya michezo yaliyoteka hisia za ulimwengu na walimwengu. Kwa kweli siku zinaenda mbio jana ilikua januari Mosi leo mwaka 2024 ni kwaheri. Kutoka AFCON hadi EURO, Olimpiki, Ndondi za uzito wa juu, Ligi ya Mabingwa CAF, na tenisi, hapa kuna habari kuu za mwaka huu:
AFCON 2024 : Mashindano ya Soka Barani Afrika
Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) lilirejea kwa burudani ya hali ya juu, likionyesha vipaji bora zaidi barani. Mwenyeji Ivory Coast walitawala, huku vigogo kama Ghana wakipata mshtuko wa kuondolewa mapema mataifa kama Cape verde yakitoa burudani ya kipekee.
CAF (Shirikisho la Soka Barani Afrika) liliripoti faida ya dola milioni 72 kutoka Mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2024. Hii inaonyesha mafanikio makubwa ya kibiashara kwa soka la Afrika katika ngazi ya kimataifa.
Kwa mwaka wa fedha wa 2024-2025, CAF inatarajia mapato ya karibu dola milioni 150, huku matumizi yakikadiriwa kuwa dola milioni 138.2, na hivyo kutabiri faida halisi ya dola milioni 11.7 – faida ya kwanza baada ya miaka kadhaa.
UEFA EURO 2024: Tamasha la Soka Ulaya
Mashindano ya UEFA EURO 2024 yalifanyika nchini Ujerumani, yakileta pamoja mataifa bora ya soka barani Ulaya. Timu ya taifa la Hispania wakawa washindi kwa kuishinda England katika fainali ushindi wa kihistoria kwa timu ambayo ilijaa wachezaji damu changa.

Olimpiki za Paris 2024: Sherehe ya Ubora wa Kimichezo
Olimpiki za Paris iliangaza majira ya joto kwa matukio ya kusisimua. Rekodi zilivunjwa, na mashujaa walijitokeza katika michezo tofauti kuanzia kwenye soka, riadha, ngumi, voliboli, basketiboli na michezo mingine mingi.
Wapenzi wa riadha kutoka bara Afrika wakiusherehekea ushindi wa wanariadha kutoka barani Afrika Letsile Tebogo kutoka Botswana, Faith Kipyegon kutoka kenya, Gudaf Tsegay, Tamirat Tola kutoka Ethiopia na Joshua Cheptegei raia wa Uganda.

Ndondi za Uzito wa Juu: Usyk Dhidi ya Fury
Mapambano ya ndondi yamekua mengi mwaka huu. Si Afrika Mashariki, si kusini mwa Afrika, si kaskazini mwa Afrika na duniani kote ila pambano la uzani wa juu lake Oleksander Usyk na Tyson Fury limechukua nafasi kubwa.
Oleksandr Usyk alithibitisha ubora wake kama mmoja wa mabondia wakubwa wa kizazi hiki kwa mara nyingine baada ya kumshinda Tyson Fury kwa pointi katika marudiano yao yaliyofanyika Riyadh, Saudi Arabia. Kwa ushindi huu wa 116-112 kutoka kwa majaji wote watatu, Usyk alidumisha mikanda yake ya WBA (Super), WBC, na WBO na kupanua rekodi yake ya kutoshindwa hadi ushindi 23 wa kulipwa.
Ligi ya Mabingwa CAF na Ligi ya Mabingwa ya Wanawake.
Soka la vilabu barani Afrika lilipanda kiwango mwaka huu, kwa kampeni za kusisimua kwenye Ligi ya Mabingwa ya CAF na Ligi ya Mabingwa ya Wanawake ya CAF.
Al Ahly SC, klabu ya soka ya Misri, ilifanikiwa kuongeza rekodi ya taji lao la 12 la Ligi ya Mabingwa wa CAF mnamo 2024. Walifanikisha hili kwa kuishinda Espérance de Tunis kwa jumla ya bao 1-0 kwenye fainali.
Ushindi huu uliimarisha zaidi ubabe wa Al Ahly katika soka la vilabu barani Afrika.
Katika mashindano ya kinadada ambayo ufanyika kwa mtindo tofauti na mashindano ya wanaume klabu ya Tp Mazembe ya kinadada iliibuka na ushindi.
All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.