Msumbiji: Kuzuka kwa ghasia kunaathiri uchumi wa nchi

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Msumbiji imekuwa ikikumbwa na mlipuko mpya wa ghasia tangu siku ya Jumatatu na na Baraza la Katiba kuthibitisha uchaguzi wa Daniel Chapo kama mkuu wa nchi. Kulingana na shirika lisilo la kiserikali la Plataforma Decide, watu 134 wameuawa tangu kuanza kwa wiki hii. Wadau wa kiuchumi wana wasiwasi juu ya shida hizi ambazo tayari zimeathiri shughuli za makampuni ya kigeni.

Kampuni ya Uingereza ya Gemfields pia ina wasiwasi kuhusu shughuli za kampuni yake tanzu. La Montepuez Ruby Mining MRM ambayo inatumia moja ya amana kubwa zaidi za rubi ulimwenguni katika mkoa wa Cabo Delgado.
Kampuni ya Uingereza ya Gemfields pia ina wasiwasi kuhusu shughuli za kampuni yake tanzu. La Montepuez Ruby Mining MRM ambayo inatumia moja ya amana kubwa zaidi za rubi ulimwenguni katika mkoa wa Cabo Delgado. AP – Carlos Uqueio

Kampuni ya uchimbaji madini ya Australia South32 bila shaka ndiyo iliyoathiriwa zaidi kwa sasa. Kichungi chake cha alumini kilichoko nje kidogo ya Maputo kimelazimika kupunguza kiwango cha uzalishaji wake. Vizuizi vingi vya barabarani vimefanya uwasilishaji wa malighafi kuwa mgumu sana.

Kampuni ya Uingereza ya Gemfields pia ina wasiwasi kuhusu shughuli za kampuni yake tanzu. La Montepuez Ruby Mining MRM ambayo inatumia moja ya amana kubwa zaidi za rubi ulimwenguni katika mkoa wa Cabo Delgado.

Uzalishaji husitishwa mara kwa mara huko kutokana na mashambulizi ya wanajihadi haswa. Na Gemfields inahofia kuvurugika, majengo kadhaa yalichomwa moto karibu na mgodi huo mapema wiki hii. “Makundi yanayohusishwa na biashara haramu ya rubi ambayo yanatumia fursa hii ya machafuko ya kisiasa,” kulingana na kampuni hii ya uchimbaji madini.

Kwa upande wa hidrokaboni – kampuni kubwa ya petrokemikali ya Afrika Kusini Sasol imepunguza uzalishaji wa gesi asilia katika kiwanda chake kikuu cha usindikaji nchini Msumbiji. Njia ya kuhakikisha usalama wa wafanyakazi na mali yake, kulingana na msemaji wake.

Afrika Kusini inategemea Msumbiji kwa uagizaji wa gesi kutoka nje. Wahusika wote hawa wanafuatilia hali hiyo kwa karibu sana, kwa hofu ya kutokea moto mkubwa ambao utaathiri vibaya zaidi uchumi wa nchi.

Barabara inayovuka nchi pia imefungwa mahali. Hivyo ni vigumu kwa mkoa wetu kupokea bidhaa, huku tunategemea sana bidhaa zinazoagizwa kutoka Afrika Kusini, ambazo lazima zipitie Maputo, amesema Arcénio Cuco, profesa huko Nampula (kaskazini mwa Msumbiji)

All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment