Rais wa AU na mwenzake wa Angola wajadili hali ya usalama nchini DRC

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Mauritania na Mwenyekiti wa sasa wa Umoja wa Afrika, Mohamed Ould Cheikh El Ghazouani, amezungumza kwa njia ya simu na mwenzake wa Jamhuri ya Angola, João Lourenço, kuhusu vipaumbele vya sasa vya Umoja wa Afrika, ikiwa ni pamoja na juhudi zinazoendelea kuhimiza amani na usalama barani humo.

Rais wa Angola, João Lourenço, mpatanishi wa Umoja wa Afrika (AU) kwa lengo la kurejesha amani mashariki mwa DRC, mjini Kinshasa, Agosti 12, 2024.
Rais wa Angola, João Lourenço, mpatanishi wa Umoja wa Afrika (AU) kwa lengo la kurejesha amani mashariki mwa DRC, mjini Kinshasa, Agosti 12, 2024. © Facebook/ Présidence de la République d’Angola

Haya ndiyo yaliyofichuliwa na Shirika la Habari la Mauritania (AMI) siku ya Alhamisi, Desemba 26, kulingana na Radio OKAPI, yenye makao yake makuu nchini DRC.

Kuhusu suala hili, Rais João Lourenço amemweleza mwenzake Ould Ghazouani, Rais wa Umoja wa Afrika (AU), kuhusu maendeleo ya mchakato wa Luanda, mpango muhimu unaolenga kurejesha utulivu mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Mazungumzo haya yanaakisi azma ya viongozi hao wawili kuchanganya juhudi zao za kushughulikia changamoto kuu zinazoikabili Afrika na kukuza ushirikiano ulioimarishwa ndani ya Umoja wa Afrika, linaongeza shirika hilo la habari la Mauritania, likinukuliwa na Radio OKAPI.

All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment