Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa
Sudan Kusini inazidiwa uwezo kutokana na wimbi kubwa la wakimbizi wanaokimbia vita nchini Sudan pamoja na mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu, hii ni kwa mujibu wa shirika la kimataifa la madaktari wasio na mipaka RSF.

Kwenye taarifa yake, shirika hilo limesema watu karibu elfu 5 wanavuka mpaka wa nchi hizo mbili kila siku, takwimu zinazouwiana na zile za umoja wa Mataifa zinazoonesha ni watu kati ya elfu 7 na elfu 10 wanavuka mpaka kila siku.
Sudan inakabiliwa na moja ya mzozo mbaya zaidi wa kibinadamu duniani uliochochewa na vita kati ya wanajeshi wa Serikali na wapiganaji wa RSF tangu mwezi April mwaka uliopita, ambapo umesababisha maelfu ya watu kuuawa na mamilioni kuwa wakimbizi.

Ofisi ya MSF nchini Sudan imetolea mfano kambi ya wakimbizi ya Renk inayohifadhi raia zaidi ya elfu 17, kuwa imezidiwa uwezo na huenda hali ikawa mbaya zaidi ikiwa msaada wa dharura hautatolewa kwa wakati.
All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.