Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa
Nchini Guinea, operesheni ya “kubomoa” “maeneo ya uhalifu” inaendelea. Ilizinduliwa tarehe 9 Desemba, inalenga kupambana na uhalifu na mauaji yaliyopangwa, kama vile biashara ya wahamiaji au biashara ya dawa za kulevya. Operesheni hii imesababisha makumi ya watu kukamatwa na kufukuzwa kwa raia wa Sierra Leone wanaoishi katika mji mkuu wa Guinea, na kusababisha mvutano kati ya nchi hizo mbili. Lakini mwendesha mashitaka anabaini kwamba operesheni hii “hailengi raia wa Sierra Leone”.

Mamlaka za Guinea zinashuku bandari za mji mkuu wa uvuvi, hasa ile ya Matam ambako wananchi wengi wa Sierra Leone wanaishi, kuwa sehemu za kupitisha bidhaa za kuagiza madawa ya kulevya. Kwa hivyo, wakati wa operesheni hiyo, raia kadhaa wa Sierra Leone walikamatwa na kupelekwa kwa nguvu mpakani, na kusababisha tukio la kidiplomasia kati ya Conakry na Freetown kwa siku kadhaa.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Guinea, Morissada Kouyaté, alimtembelea rais wa Sierra Leone siku ya Jumanne. Julius Maada Bio alimweleza wasiwasi wake kuhusu kudhulumiwa kwa raia wake nchini Guinea.
Tangu wakati huo, mwendesha mashtaka wa Mahakama ya Rufaa ya Conakry amekanusha kulengwa kwa raia wa Sierra Leone. Kulingana na chanzo cha mahakama, polisi waliwakamata wahalifu ambao walitoka Sierra Leone.
Kwa hali yoyote, tukio hilo haliitii shaka operesheni ambayo inapaswa kuendelea angalau hadi mwisho wa mwezi. Kulingana na mwendesha mashtaka, kuna zaidi ya maeneo 400 “ya uhalifu” ambayo yanaweza kubomolewa katika wilaya 13 za Conakry. Baada ya hapo, itaendelea katika miji mikuu mingine ya kikanda kama vile Kindia, Boké na Mamou.
All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.