Kisa cha kwanza kibaya cha maambukizi ya mafua ya ndege chagundulika Marekani

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Kisa cha kwanza kibaya cha maambukizi ya virusi vya H5N1 kimegunduliwa nchini Marekani, mamlaka ya Marekani imetangaza hivi punde siku ya Jumatano, wakati hofu ya uwezekano wa mlipuko wa homa ya mafua ya ndege ikiongezeka.

Homa ya mafua ya ndege kwa ujumla ni ya msimu lakini katika miaka ya hivi karibuni kesi zimeonekana mwaka mzima.
Homa ya mafua ya ndege kwa ujumla ni ya msimu lakini katika miaka ya hivi karibuni kesi zimeonekana mwaka mzima. © JEAN-PIERRE MULLER / AFP

Mgonjwa huyo, aliyelazwa katika hospitali ya Louisiana (kusini), ni kisa cha 61 cha binadamu cha mafua ya ndege kugunduliwa tangu mwezi Aprili nchini humo, Kituo cha Marekani cha Kuzuia na Kudhibiti Magonjwa (CDC) kimesema katika taarifa yake kwa vyombo vya habari.

Akiwa na umri wa zaidi ya miaka 65 na anaugua magonjwa mengine, yuko katika “hali mbaya” na “anaugua ugonjwa mbaya wa kupumua”, mamlaka ya afya ya Louisiana imelielezea shirika la habari la AFP.

Watu wengine walioambukizwa walikuwa na dalili kali.

Kwa miezi kadhaa, Marekani imekuwa ikikabiliwa na mlipuko – sawa na janga kati ya wanyama – ya mafua ya ndege.

Vipengele kadhaa vinapendekeza kwamba “homa ya mafua ya ndege inagonga mlango wetu na inaweza kusababisha janga jipya”, Meg Schaeffer, mtaalam wa magonjwa katika taasisi ya SAS ya Marekani, ameliambia shirka la habari la AFP hivi karibuni.

Walakini, mamlaka ya afya ya Marekani imehakikisha Jumatano kwamba tathmini yao ya hatari iliyotolewa na homa ya mafua ya ndege kwa afya ya umma haikubadilika na imebaki “chini”.

“Kuenea kwa Homa ya mafua ya ndege (aina ndogo) H5 kutoka kutoka kwa maabukizi ya binadamu hakujagunduliwa,” wamesema.

Kesi zingine mbaya za Homa ya mafua ya ndege kwa wanadamu tayari zimegunduliwa katika nchi zingine, mamlaka ya afya ya Marekani imekumusha. Hii ni hasa kisa cha kijana aliyelazwa hospitalini mnamo Novemba katika mko wa Canada wa British Columbia (magharibi).

– Mabadiliko ya virusi –

Mtafiti katika Chuo Kikuu cha Jimbo la Louisiana, Rebecca Christofferson amelieleza shirikala habari la AFP kwamba kutokana na kukosekana kwa ufuatiliaji wa kina, ilikuwa vigumu kujua kama maambukizi kutoka kwa wanyama kwenda kwa binadamu ulikuwa ukiongezeka mara kwa mara au ikiwa maambukizi kati ya binbadamu yasiyo na dalili yalikuwa yakitokea.

“Sina hofu bado,” hata hivyo amefafanua, huku akisisitiza haja ya kuongezeka kwa uangalifu.

Kulingana na CDC, mgonjwa huyo wa Louisiana aliwasiliana na ndege wagonjwa na waliokufa kwenye ua.

Mfuatano wa genomic ulionyesha kuwa virusi vya H5N1 vilivyomwambukiza ndivyo vilivyoambukiza watu katika jimbo la Marekani la Washington na nchi jirani ya Canada, pamoja na ndege wa porini na kuku nchini Marekani.

Toleo hili la H5N1 ni tofauti na lile linalogunduliwa kwa ng’ombe na vile vile katika kesi za kibinadamu na kuku wengine.

Virusi vya homa ya mafua ya ndege vinasambaa nchini Marekani katika mashamba ya kuku na vimekuwa vikienea kwa njia ambayo haijawahi kushuhudiwa tangu mwezi Machi katika makundi ya ng’ombe.

Na mwishoni mwa mwezi wa Oktoba, nguruwe katika shamba la Oregon ambaye pia alikuwa akihifadhi kuku na mifugo alipatikana na virusi vya H5N1, ingawa hakuonyesha dalili za ugonjwa.

Kutokana na kuenea kwa visa vya homa ya ndege kwenye mashamba yake ya mifugo, California imechukua hatua za dharura ili mashirika ya serikali yawe na uhuru wa “kujibu haraka”, ametangaza gavana wake Gavin Newsom Jumatano.

– Kugusa wanyama walioambukizwa –

Kuongezeka kwa idadi ya mamalia walioambukizwa na ugonjwa huo kunatia wasiwasi wataalam ambao wanahofia kwamba mzunguko mkubwa unaweza kuwezesha mabadiliko ya virusi ambayo ingeruhusu kupita kutoka kwa mwanadamu mmoja hadi mwingine.

Ugunduzi wa hivi majuzi wa mafua ya ndege kwa watu ambao hawajagusana na mnyama aliyeambukizwa huimarisha wasiwasi katika suala hili.

Takriban watu watatu wameambukizwa katika miezi ya hivi karibuni na virusi vya H5N1 nchini Marekani bila kujua asili ya kuambukizwa kwao.

Wakati athari za virusi hivyo zimegunduliwa kwenye maziwa mabichi au ambayo hayajasafishwa, Idara ya Kilimo ya Marekani imetangaza siku ya Jumatano mpango mpya unaolenga kuimarisha uchunguzi katika eneo hili.

Kuna mashaka juu ya jinsi utawala wa Rais mteule Donald Trump utakabili mlipuko huo. Waziri wa Afya aliyechaguliwa na Bw. Trump, Robert Kennedy Jr, ni mfuasi maarufu wa maziwa mabichi.

Kulingana na takwimu zilizotajwa Jumanne huko Geneva na afisa kutoka Shirika la Afya ya Wanyama Duniani, Gregorio Torres, mlipuko wa Homa ya mafua ya ndege umesababisha vifo vya ndege zaidi ya milioni 300 kote ulimwenguni tangu mwezi Oktoba 2021.

Katika miaka mitatu, virusi vya H5N1 vimegunduliwa katika nchi au wilaya 108 kwenye mabara matano na katika zaidi ya spishi 70 za mamalia, wa nyumbani au wa porini.

All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment