Msumbiji: Kimbunga Chido chaua takriban watu 34

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Kimbunga Chido kimeua takriban watu 34, kujeruhi zaidi ya 300 na kuharibu zaidi ya nyumba 20,000 nchini Msumbiji, Taasisi ya Kitaifa ya Kudhibiti Hatari na Majanga imetangaza siku ya Jumanne Desemba 17, 2024.

Watu 175,000 wameathiriwa kufuatia Kimbunga Chido nchini Msumbiji.
Watu 175,000 wameathiriwa kufuatia Kimbunga Chido nchini Msumbiji. © AFP

Kimbunga hicho, ambacho kiliharibu visiwa vya Ufaransa vya Mayotte siku ya Jumamosi, kisha kupiga jimbo la Msumbiji la Cabo Delgado siku ya Jumapili, ambapo watu 28 wameuawa, kulingana na taasisi hiyo. Wengine watatu walifariki katika jimbo la Nampula na wengine watatu katika jimbo la Niassa, bara, Taasisi ya Kitaifa ya Kudhibiti Hatari na Majanga imeongeza.

Taasisi hiyo pia imehesabu majeruhi 319 wakati wa kimbunga hicho kimekuwa kikipita, ambacho upepo wake ulifikia kilomita 260 kwa saa na mvua ya milimita 250 katika saa 24. Karibu nyumba 23,600 na boti 170 za uvuvi ziliharibiwa, ameongeza. Watu 175,000 wangeathiriwa na janga hilo.

Kimbunga Chido kimekumba eneo la kaskazini mwa Msumbiji ambalo halijaendelea, ambalo mara kwa mara hukumbwa na vimbunga na tayari linakabiliwa na migogoro. Kimunga Chido kilielekea Malawi siku ya Jumatatu, na kinatarajiwa kutoweka karibu na Zimbabwe siku ya Jumanne.

Huko Mayotte, katika Bahari ya Hindi, viongozi wanahofia vifo vya “mia kadhaa” baada ya kupita kwa kipmbunga Chido, labda hata “maelfu”. Chido ndicho kimbunga kikali zaidi ambacho Mayotte, idara maskini zaidi ya Ufaransa, imepitia katika miaka 90. Imeainishwa katika kategoria ya 4 (kati ya 5), ​​siku ya Jumamosi ilivuka moja kwa moja kupitia visiwa vidogo ambako karibu theluthi moja ya wakazi wanaishi katika makazi hatarishi.

All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment