Niger yasitisha matangazo ya BBC kwa miezi mitatu na kuwasilisha malalamiko dhidi ya RFI

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Mamlaka ya Niger imesitisa matangazo ya redio ya BBC kwa miezi mitatu. Kituo cha redio kinachozungumza Kiingereza kinashutumiwa kwa kuchapisha, kwa mujibu wa mamlaka, ripoti zisizo rasmi kuhusu mashambulizi ya hivi punde nchini humo. Kusitishwa huko kunahusu kutajwa kwa shambulio la kijiji cha Chatoumane ambalo lilisababisha vifo vya zaidi ya watu mia moja; shambulio ambalo mamlaka ilikanusha siku ya Jumatano jioni, ikitoa “madai yasiyo na msingi”. 

Jenerali Abdourahamane Tiani, Julai 6, 2024 mjini Niamey.
Jenerali Abdourahamane Tiani, Julai 6, 2024 mjini Niamey. © Mahamadou Hamidou / Reuters

Kufuatia mkutano wa Baraza la Mawaziri, serikali imetangaza katika taarifa kwa vyombo vya habari kwamba inawasilisha malalamiko dhidi ya RFI.

Katika taarifa yake ya adhuhuri, BBC Africa ilitangaza kwamba “wapiganaji wanaoshukiwa walianzisha mashambulizi mawili kwa wakati mmoja katika kijiji cha Chatoumane na katika eneo la Téra” na pia kusababisha vifo vya watu 130. Haikuchukua muda mrefu kwa mamlaka kusitisha matangaz ya redio hiyo kwa miezi mitatu.

BBC inashutumiwa kwa kutangaza “habari potofu zinazoelekea kuvuruga utulivu wa kijamii na kudhoofisha ari ya wanajeshi wanaopigana dhidi ya wanajihadi”, kulingana na taarifa kwa vyombo vya habari kutoka kwa Waziri wa Mawasiliano, Sidi Mohamed Raliou.

Siku ya Jumatano jioni, makao makuu ya jeshi ilithibitisha kwenye televisheni ya umma kukanusha rasmi kuhusu shambulio la Chatoumane na kutangaza kwamba hayo yalikuwa “madai yasiyo na msingi” na “kampeni ya ulevi iliyopangwa na wapinzani wa watu wa Niger kwa lengo la kudhoofisha maadili ya askari wetu na kuchochea mgawanyiko kati ya raia na mashujaa wetu wa FDS.

Kulingana na vyanzo vya usalama na vya hospitali, askari wasiopungua 90 waliuawa, pamoja na karibu raia hamsini waliokwama katika mapigano.

Tangu mapinduzi ya kijeshi ya mwezi Julai 2023, vyombo vya habari na waandishi wa habari nchini Niger wamekabiliwa na matatizo katika kutekeleza taaluma yao. Wiki moja baada ya Mohamed Bazoum kuchukua mamlaka, matangazo ya RFI na France 24 yalisitishwa nchini Niger na hadi leo hatua hiyo haijaondolewao.

Utawala wa Niger pia umetangaza siku ya Alhamisi jioni “kuwasilisha malalamiko” dhidi ya RFI, inayoshutumiwa kwa “kuandaa” “kampeni kubwa ya upotoshaji”, inabainisha taarifa kwa vyombo vya habari kutoka Baraza la Mawaziri la Desemba 12.

All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment