Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa
Nchini Mali, mji wa Léré umekuwa chini ya vizuizi vya wanajihadi kwa wiki mbili sasa. JNIM (kundi linalodai kutetea Uislamu na Waislamu), lenye uhusiano na Al-Qaeda, kimetoa marufuku mnamo Novemba 29 kwenye eneo hili katika eneo la Timbuktu, lililoko karibu kilomita sitini kutoka Mauritania. Mkakati ambao tayari umetekelezwa mara kadhaa katika maeneo mbalimbali, katikati na kaskazini mwa Mali: mwaka mmoja uliopita hasa, jiji la Timbuktu lenyewe lilikuwa chini ya kizuizi kikubwa.
Kuanzia sasa na kuendelea, ni ufikiaji wa Léré ambao umetatizwa sana na wanajihadi, hali ambayo ina athari huko Timbuktu.
“Malori yalienelea kuzuiliwa kwenye lango la mji, baadhi yamerudi nyuma” wanashuhudia wakazi kadhaa, kutoka Léré yenyewe au kutoka eneo hilo.
Kulingana na msafirishaji anayefanya kazi katika eneo hilo, barabara inayounganisha Léré na Niono na, zaidi, hadi Bamako, imekatwa kabisa. hali kama hiyo kwa malori yanayotoka Mauritania: “tunapaswa kusafirisha bidhaa kwa njia ya mto kutoka Mopti”, anashuhudia msafirishaji huyu, ambaye anaongeza kuwa kuongezeka kwa maji kunasababisha hali kuwa ngumu zaidi. Ushuhuda uliokaguliwa na vyanzo vingi vya ndani, ambavyo vinaelezea “kizuizi kamili”.
Malori kutoka Algeria, hata hivyo, yangeweza kuingia Léré, kulingana na baadhi ya vyanzo. Hakuna uhaba mjini, lakini shuhuda zinaripoti bidhaa nyingi zinazokosekana – maziwa, pasta, mafuta – pamoja na ongezeko la bei. Vizuizi vilivyowekwa na wanajihadi wa JNIM pia vina athari kwa mji mkuu wa mkoa, Timbuktu: sio kwa usambazaji, lakini kwa shughuli za wakaazi. “Hii imepunguza sana usafiri wa mabasi,” anashuhudia mtu mashuhuri kutoka Timbuktu.
All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.