Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa
Nchini Nigeria genge la watu wenye silaha limewateka zaidi ya wanawake 50 wakiwemo watoto katika kijiji cha Kakin Dawa, katika jimbo la Zamfara Kaskazini Magharibi mwa nchi hiyo.

Polisi na wakaazi wamesema, uvamizi huo utekelezwa Jumapili iliyopita, na watekaji wanadai kikombozi ili kuwaachia huru mateka hao.
Aidha, wakaazi wa kijiji cha Kakin Dawa, wamesema, watu hao wente silaha walikuwa kwenye pikipiki wakati walipotekeleza uvamizi huo.
Wakiwa wamejihami kwa silaha, walipita na kuingia nyumba kwa nyumba, wakitekeleza uhalifu huo kwa mujibu wa polisi na wakaazi hao.
Polisi katika êneo la Zamfara wamesema vikosi vya ziada tayari vimetumwa eneo hilo kuweka usalama ,wakati huu raia wakiomba vyombo vya usalama kutuma askari zaidi.
Kwa zaidi ya miaka 15 êneo la kaskazini magharibi mwa Nigeria limekumbwa na ukosefu kutokana na uvamizi wa makundi ya kiislamu yanayotaka kujitenga, huku utekaji nyara kwa ajili ya fidia ukiongezeka êneo hilo kutokana pia na umasikini, ukosefu wa ajira na silaha kuwa mikononi mwa watu.
All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.