Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa
Kiongozi wa kikosi cha kudumisha Amani, cha umoja wa mataifa, nchini DRC, Bintou Keita, amewataka wanasiasa na mashirika ya kiraia nchini humo kutochochea hali ya wasi wasi nchini humo.
Akihubia kikao cha baraza la usalama la umoja wa mataifa jijini New York, Bintou Keita, amekiri hali ya usalama imezidi kuzorota eneo la Kivu Kaskazini tangu mwaka jana, hali hiyo ikichangiwa na mapigano ya makundi ya ya waasi wa ADF, M23, CODECO na Zaire.

Hata hivyo amesema joto la kisiasa linalochangiwa na mjadala kuhusu marekebisho ya katiba, mjadala ulionzishwa na rais Felix Tshisekedi , linachangia hali ya taharuki.
Amewataka wanasiasa na viongozi wa mashirika ya kiraia kushirikiana na kuendesha mazungumzo kuhusu swala hilo kwa amani ili kutozidisha hali ya wasi wasi.
Bintou Keita amelisisitizia baraza hilo kuunga mkono mikakati ya kurejesha amani nchini DRC, ikiwemo ukamataji silaha .
All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.