CAR: Waendesha mashtaka waiomba ICC kuwahukumu viongozi wa wanamgambo

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Waendesha mashtaka katika mahakama ya kimataifa ya kushughulikia uhalifu wa kivita, ICC wameitaka mahakama hiyo kuthibitisha kesi dhidi ya viongozi wawili wa kundi la waasi nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, lilofahamika kama anti-Balaka.

Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) The Hague
Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) The Hague REUTERS – Jerry Lampen

Waendesha mashtaka katika mahakama ya kimataifa ya kushughulikia uhalifu wa kivita, ICC wameitaka mahakama hiyo kuthibitisha kesi dhidi ya viongozi wawili wa kundi la waasi nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, lilofahamika kama anti – Balaka.

Wanamgambo wa Anti-balaka huko Gamba, kusini-mashariki mwa CAR mnamo 2017
Wanamgambo wa Anti-balaka huko Gamba, kusini-mashariki mwa CAR mnamo 2017 AFP / Alexis Huguet

Wakitia hoja zao za mwisho katika kesi dhidi ya wawili hao ilionza mwaka 2021, waendesha mashtaka hao, wamesema wana uthibitisho tosha kuwa wawili hao Patrice Edourd Ngaissona na Alfred Yekatom, waliongoza kampeni ya machafuko yaliyolenga raia waislamu.

Mwendesha mashtaka Kweku Vanderpuye, alitupilia mbali utetezi wa upande wa Ngaissona, uliodai kuwa kiongozi huyo wa waasi wa anti Balaka, pia mchezaji wa mpira wa mguu, alijaribu kumaliza machafuko hayo.

Wanajeshi wa kikosi cha Umoja wa Afrika (Misca) katika kata ya Boy-rabe, makao makuu ya wanamgambo wa anti-balaka, mjini Bangui, februari 19 mwaka 2014 ...
Wanajeshi wa kikosi cha Umoja wa Afrika (Misca) katika kata ya Boy-rabe, makao makuu ya wanamgambo wa anti-balaka, mjini Bangui, februari 19 mwaka 2014 … FRED DUFOUR/AFP

Upande wa mashtaka pia ulisema kuwa Yekatom aliyefahamika kwa jina la Rambo alikuwa kiongozi wa waasi hao zaidi ya elfu tatu aliogopwa mno katika kundi hilo, akiwa amewapiga risasi na kuwauwa wapiganaji Wake watatu waliotuhumiwa kuwa wasaliti. Wawili hao hata hivyo walikanusha mashtaka hayo dhidi yao mwaka 2021.

Waasi wa anti-Balaka walianzisha mapigano mwaka 2013 kujibu mauaji na uporaji uliokuwa ukiendesha na waasi wa kislamu wa Seleka waliokuwa wamechukua uongozi mwaka huo.

Wanamgambo wa Anti-balaka huko Bambari,nchini CAR mnamo 2014
Wanamgambo wa Anti-balaka huko Bambari,nchini CAR mnamo 2014 AFP / Andoni Lubaki

ICC imekuwa ikichunguza uhalifu wa kivitua nchini Jamhuri ya Kati tangu mwaka 2014 na kuna kesi inayoendelea pia dhidi ya kiongozi wa waasi wa Seleka.

All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment