Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa
Mahakama ya kijeshi kwenye mji wa Ndolo nchini DRC, imethibitisha adhabu ya kifo waliyopewa washirika watano wa aliyewahi kuwa mwenyekiti wa tume ya uchaguzi nchini humo, Corneille Nangaa, ambaye kwa sasa anaongoza vuguvugu la Alliance Fleuve Congo.

Katika kesi hio, wahusika watano waliopewa hukumu hiyo ni Eric Nkuba Shebandu, Samafu Makinu Nicaise, Nangaa Baseyane Ruttens, M’Kangya Nyamatshaba na Safari Bishori Luc.
Kulingana na hukumu, watano hao, walipatikana na makosa ya uhalifu wa kivita, mauaji ya kukusudia, uharibifu wa mali na ushiriki katika harakati za uasi uliofanywa na wasaidizi walio chini ya mamlaka yao.
Hata hivyo wataalamu wa sheria wanasisitiza kuwa, ingawa hukumu ya kifo imethibitishwa, bado kuna njia ya kupinga kupitia rufaa mbele ya Mahakama ya juu.
Aidha Corneille Nangaa na wenzake 20 ambao walihukumiwa bila kuwepo mahakamani, wataendelea kusubiri baada ya Mahakama Kuu ya Kijeshi Kusitisha mchakato wa rufaa dhidi yao.
All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.