Chuma Hunoa Chuma,Umejifunza nini kwa Tajiri na Mvuvi?

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Siku moja tajiri mmoja alienda baharini (Beach) kupunga upepo.

Wakati akitembea huku na kule akiwaza na kuwazua juu ya biashara zake, mara ghafla akamwona mvuvi mmoja amekula zake tano

😎

 (amelala chali na kuota jua) na mtumbwi wake pembeni imejaa samaki.

Tajiri akamsogelea na kumwambia……

Tajiri: Wewe Mbona unalala SASA hivi, amka ukavue samaki, uuze ili upate hela?

Mvuvi: Ili iweje?

Tajiri: Uwe na pesa nyingi uajiri watu wakusaidie kuvua samaki.

Mvuvi: Ili iweje?

Tajiri: Biashara YAKO iwe kubwa na uwe ununue meli uanze kusafirisha nje ya nchi.

Mvuvi: Ili iweje?

Tajiri: Uwe na hela nyingi, uwe unakuja tu bahari kupumzika na kupunga upepo kama Mimi.

Mvuvi: Kwani hapa nafanyaje?

Umejifunza nini kwa Tajiri na Mvuvi?

All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment