Namibia: Kiongozi mkuu wa upinzani atoa wito wa kufutwa kwa uchaguzi

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Mpinzani mkuu nchini Namibia ameonya kuwa hatatambua matokeo ya uchaguzi wenye machafuko uliomalizika Jumamosi baada ya siku nne za upigaji kura katika nchi hiyo ya jangwa kusini mwa Afrika. Hata kama matokeo ya uchaguzi huu yalikuwa mazuri kwake.

Mgombea urais wa chama cha upinzani cha IPC Panduleni Itula, Novemba 29, 2024 mjini Windhoek, Namibia.
Mgombea urais wa chama cha upinzani cha IPC Panduleni Itula, Novemba 29, 2024 mjini Windhoek, Namibia. © Noah Ndero Tjijenda / REUTERS

Mgombea urais Panduleni Itula, ambaye alishika nafasi ya pili mwaka wa 2019, alionya kwamba chama chake “hakitatambua matokeo” ya chaguzi hizi, saa chache kabla ya kutangazwa kwa sehemu ya matokeo yanayotarajiwa na kufungwa kwa uhakika kwa vituo vichache vya kupigia kura vilivyofunguliwa upya.

Mbele ya kituo katika mji mkuu Windhoek, zoezi la  kuhesabu kura lilicheleweshwa kuanza baada ya mpiga kura wa mwisho kupiga kura muda mfupi baada ya 3:00 usiku saa za nchini hiyo.

Panduleni Itula alitangaza kwa vyombo vya habari kwamba ana nia ya kutaka uchaguzi huu ambao haujaamuliwa kwa chama cha kihistoria kilichopo madarakani “kufutwa” kulingana na “taratibu zilizowekwa”, “licha ya matokeo yoyote”.

“Hatuwezi kuelezea uchaguzi huu kama huru, wa haki na halali,” alikashifu mpinzani huyo baada ya matukio siku ya Jumatano, wakati baadhi ya Wanamibia walilazimika kusubiri hadi saa 12 kupiga kura.

Ikiongozwa na chama hicho, SWAPO, tangu uhuru wake mwaka 1990, Namibia, ambayo inajivunia amani na demokrasia yake, inaingia kwenye mgogoro mbaya zaidi wa kitaasisi. Itula, daktari wa meno na mwanasheria wa zamani mwenye umri wa miaka 67, alitoa wito kwa Rais Nangolo Mbumba “kukutana na baraza lake la mawaziri ili kuamua nini kifanyike”.

Uchaguzi uliofunguliwa siku ya Jumatano, kumchagua rais na Bunge, uliongezwa mara mbili baada ya mistari kuwa tuli kwani haikuwa na kikomo jambo ambalo liliwazuia wapiga kura wengi, kati ya milioni 1.5 waliojiandikisha, kupiga kura zao.

“Michakato ya upigaji kura ilicheleweshwa kwa makusudi katika zaidi ya 63% ya vituo vya kupigia kura nchini,” kulingana na ripoti ya Shirika la Wanasheria wa Haki za Kibinadamu Kusini mwa Afrika, ambalo lilituma ujumbe wa uchunguzi.

Ujumbe huu, uliyosambazwa kote nchini, pia umeripoti “kucheleweshwa kwa makusudi katika kuwasili kwa kadi za kupigia kura”.

All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment