Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa
Rais wa Kenya William Ruto amesema siku ya Jumamosi yeye na Rais wa Uganda Yoweri Museveni watasaidia kupatanisha Ethiopia na Somalia katika mzozo unaotishia kuvuruga ukanda wa Pembe ya Afrika.
Ethiopia isiyo na bandari, ambayo ina maelfu ya wanajeshi nchini Somalia kupambana na waasi wenye mafungamano na al Qaeda, imeikasirisha serikali ya Mogadishu kwa mpango wake wa kujenga bandari katika eneo lililojitenga la Somaliland.
Somaliland, ambayo badala ya bandari hiyo inaweza kupata kutambuliwa kama taifa huru kutoka Ethiopia, imejitahidi kupata kutambuliwa kimataifa licha ya kujitawala na kufurahia amani na utulivu linganishi tangu kujitangazia uhuru wake mwaka 1991.
Mzozo huo umeifanya Somalia kuwa karibu na Misri, ambayo imekuwa ikizozana na Ethiopia kwa miaka mingi juu ya ujenzi wa Addis Ababa wa bwawa kubwa la maji kwenye Mto Nile, na Eritrea, adui mwingine wa Ethiopia.
“Kwa sababu usalama wa Somalia … unachangia pakubwa kwa uthabiti wa eneo letu, na mazingira ya wawekezaji na wafanyabiashara na wafanyabiashara kustawi,” Ruto amesema katika mkutano na waandishi wa habari kwenye mkutano wa wakuu wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).
Majaribio kadhaa ya kutatua mzozo mjini Ankara, Uturuki, yameshindwa kufanikiwa.
Ofisi ya Rais wa Somalia Hassan Sheikh Mohamud imesema katika taarifa kwamba Mohamud alikutana na Ruto na Museveni kando ya mkutano huo, lakini haikuzungumzia upatanishi unaowezekana.
Ahmed Moallim Fiqi, Waziri wa Mambo ya Nje wa Somalia, ameliambia shirika la habari la REUTRES kuwa maazimio ya awali ya viongozi wa kanda hayakuwa na mashiko mjini Addis Ababa, lakini ana imani juhudi za upatanishi zinazoendelea kufanywa na Uturuki zitakuwa na manufaa.
All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.