Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa
Chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania, Chadema, kimeshutumu mauaji ya wafuasi wake wawili katika mkesha wa uchaguzi wa serikali za mitaa siku ya Jumatano, na kuishutumu serikali kwa udanganyifu katika uchaguzi wa sasa.

Uchaguzi huu unachukuliwa na waangalizi wengi kama kipimo cha kidemokrasia katika mazingira ya kuongezeka kwa ukandamizaji wa kisiasa katika miezi ya hivi karibuni katika nchi hii ya Afrika Mashariki, kabla ya uchaguzi wa urais na wabunge mwaka ujao.
Huu pia ni uchaguzi wa kwanza tangu kuingia madarakani kwa Samia Suluhu Hassan, ambaye kama makamu wa rais wa John Magufuli, aliyefariki dunia ghafla Machi 202, alirithi nafasi yake. Mkuu huyo wa nchi alitangaza katika hotuba yake siku ya Jumanne kwamba serikali imedhamiria “ kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa uwazi na haki”.
Takriban wapiga kura milioni 31 wameitwa kupiga kura ili kuwateua zaidi ya viongozi 80,000 watakaochaguliwa kutoka miji, vijiji na vitongoji kote nchini. Wakati upigaji kura ukiendelea siku ya Jumatano, chama cha Chadema kimetangaza kuwa mmoja wa wagombea wake na ofisa wa ndani wa chama waliuawa siku moja kabla.
Chama hicho kimesema mgombea wake George Juma aliuawa kwa kupigwa risasi na polisi akiwa nyumbani kwake mkoani Manyoni, katikati mwa nchi, na kwamba kiongozi wa chama hicho katika Jimbo la Tunduma (Kusini Magharibi) Steven Chalamila alifariki dunia baada ya kushambuliwa kwa mapanga akiwa nyumbani kwake. “Tunalaani mauaji yote ambayo yametokea na tunatoa wito kwa polisi kufanya kile kinachohitajika ili kuwakamata na kuwafikisha wahusika mbele ya vyombo vya sheria,” chama kimeandika.
Polisi walithibitisha kifo cha George Juma, lakini walisema aliuawa kwa “risasi za onyo hewani” kutoka kwa walinzi wa gereza jirani ambao waliingilia kati mgogoro kati ya wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), chama tawala na CHADEMA.
“Kura zilizowekwa zilizopigwa mapema”
Chadema nayo inasema imebaini matukio ya utapeli kwa madai kuwa maafisa wake wamekuta masanduku ya kura yaliyojazwa mapema kura kwa faida ya CCM katika majimbo yasiyopungua matano, lakini yalikamatwa na polisi walipojaribu kuingilia kati. Chama “kinadai” wizara yenye dhamana ya serikali za mitaa “itoe ufafanuzi kwa umma kuhusiana na kadi za kupigia kura kwa wagombea wa CCM katika maeneo mbalimbali nchini.”
Kwa miezi kadhaa, upinzani, ambao ulisusia uchaguzi uliopita wa mwaka 2019, umelaani kukithiri kwa ukandamizaji dhidi yao. Unamtuhumu Samia Suluhu Hassan ambaye alionyesha dalili za uwazi wakati anaingia madarakani, kurejea kwenye mienendo ya kimabavu ya mtangulizi wake John Magufuli (watu kukamata, kutekwa n.k) wakati muda wa mwisho wa uchaguzi ukikaribia.
Chadema kinadai kuwa kimeweza tu kuwasilisha wagombea kwa theluthi moja ya viti, wakati CCM, inayotawala tangu uhuru mwaka 1961, ipo chi nzima. Akikamatwa mara kadhaa katika miezi ya hivi karibuni, kiongozi wake mkuu Freeman Mbowe alikamatwa tena kwa muda mfupi siku ya Ijumaa jioni, akiwa na viongozi wengine wa Chadema, Magharibi mwa nchi, baada ya polisi kutawanya moja ya mikutano yake.
Chadema pia inavituhumu vyombo vya ulinzi na usalama kuhusika na upotevu wa wanachama wake kadhaa na katika mauaji ya Ali Mohamed Kibao, mmoja wa viongozi wake aliyekutwa amefariki Septemba 7.
All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.