Maeneo 10 Makubwa Yanayoleta Migogoro Kwenye Ndoa Kuhusu Pesa.

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Kwa WANANDOA Wanaotaka Mafanikio Ya KIFEDHA…

i. Tofauti ya Vipaumbele

ii. Tofauti ya Mitazamo Ya Kipesa

iii. Ndugu wa Karibu

iv. Watoto wa Nje

v. Matumizi ya Kificho

vi. Mikopo ya Kificho

vii. Kushuka kwa Kipato

viii. Majukumu kwa Wazazi

ix. Uwekezaji Kwenye Biashara / Kampuni / Wazo

x. Ugonjwa

Katika Makala Hii Tutazungumzia Eneo la Saba

– Kushuka Kwa Kipato

Kama watu wamezoea maisha ya aina fulani halafu ghafla kipato kikabadilika na kikawataka kubadilisha baadhi ya vitu kama vile:

Aina ya nyumba wanayoishi, shule wanazosoma watoto etc.

Mambo haya huanza kuleta “stress” katika mahusiano na huweza kupelekea ugomvi mkubwa.

Mara nyingi katika nyakati hizi, mahitaji huwa ni makubwa na kipato cha kumudu huwa ni kidogo.

Hivyo kila pesa inapojadiliwa huwa ni kwa sababu haitoshi.

Na husababisha mazungumzo yawe na msuguano mkubwa sana.

Hii ndio maana mara kipato cha wanandoa kinaposhuka lazima kuwe na majadiliano ya namna ya kubadilisha mfumo wa maisha wa wahusika.

All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment