Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa
Jeshi la Israel linaendelea na mashambulizi yake makali ya mabomu katika viunga vya kusini mwa Beirut, na pia kusini mwa Lebanoni ambapo linasema linalenga maeneo ya Hezbollah. Wakati huo huo, imepanua operesheni zake za ardhini kusini-mashariki mwa nchi. Wakati wa mazungumzo ya simu, Joe Biden amemwomba Benyamin Netanyahu “kupunguza athari kwa raia” nchini Lebanon, haswa huko Beirut, huku “akithibitisha haki ya Israeli ya kulinda raia kutokana na mashambulizi ya Hezbollah”.

Unachotakiwa kujua
► Jeshi la Israel limeanzisha mashambulizi manne ya ardhini karibu kwa wakati mmoja katika maeneo tofauti kwenye mpaka na Lebanoni kwa lengo la wazi la kuteka vilima nane. Kutoka pwani ya Mediterania hadi Golan inayokaliwa na sehemu ya kusini mwa Lebanoni na kuwapa wakazi wao faida fulani.
► Ulipizaji kisasi kwa Israeli dhidi ya Iran baada ya shambulio lake la makombora litakuwa ” baya, sahihi na la kushangaza “, alitangaza Yoav Gallant, Waziri wa Ulinzi wa Israeli siku ya Jumatano jioni kwenye video.
► Takriban Wapalestina 16 waliuawa kaskazini na katikati mwa Ukanda wa Gaza katika mashambulizi ya Israel, hasa huko Jabalia, siku Jumatano, limeripoti shirika la habari la Palestina WAFA. Idara ya huduma za dharura zimeripoti vifo 18 usiku Jumanne kuamkia Jumatano.
► Joe Biden, Kamala Harris na Benjamin Netanyahu walizungumza kwa njia ya simu siku ya Jumatano kuhusu mvutano na Iran, hali ambayo inatishia vita vikubwa, na mzozo unaoendelea na Lebanoni. Rais wa Marekani amemtaka Netanyahu “kupunguza athari kwa raia” nchini Lebanoni, hasa huko Beirut, huku “akithibitisha haki ya Israel ya kuwalinda raia wake kutoka kwa Hezbollah.”
All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.