Uganda kuweka sheria ya kuheshimu wazee

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://liveonlineradio.net/radio-fortune-africa

Kulingana na Sensa ya Watu na Makazi ya Uganda iliyohitimishwa Juni 2024, watu wenye umri wa miaka 60 na zaidi ni asilimia 5 ya idadi ya watu nchini humo—takriban watu milioni 2.3.Serikali ya Uganda inapanga kuwasilisha sheria inayolenga kurejesha heshima na maadili kwa wazee / Picha: Reuters

Serikali ya Uganda inapanga kuwasilisha sheria inayolenga kurejesha heshima na maadili kwa wazee, ikitaja wasiwasi kwamba vizazi vichanga, vilivyoathiriwa na tamaduni za magharibi, vinazidi kupuuza hekima na mwongozo wa wazee wao.

Hayo yamebainishwa na Dominic Mafwabi Gidudu, Waziri wa Nchi anayeshughulikia Wazee, wakati akitoa taarifa Bungeni kuelekea Siku ya Kimataifa ya Wazee inayotarajiwa kufanyika Oktoba 1, 2024.

“Kuna changamoto inayoongezeka ya kizazi cha vijana kushindwa kuthamini mwongozo na hekima ya wazee, hasa kutokana na ushawishi wa kisasa na utamaduni wa Magharibi,” ameongezea.

Amesema Wizara ya Jinsia, Kazi, na Maendeleo ya Jamii inashirikiana na Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuimarisha kanuni za Muswada wa Sheria ya Wazee. Hii ikiwa na nia ya kurejesha maadili na kuhakikisha heshima kwa wazee, hasa katika utoaji huduma.

Kulingana na Sensa ya Watu na Makazi ya Uganda iliyohitimishwa Juni 2024, watu wenye umri wa miaka 60 na zaidi ni asilimia 5 ya idadi ya watu nchini humo—takriban watu milioni 2.3.

Katika kukabiliana na changamoto zinazoongezeka kwa wazee, Wizara ya Jinsia imetangaza mipango ya kuanza kudhibiti makazi ya wazee, sawa na jinsi nyumba za watoto zinavyodhibitiwa.

Gidudu aliangazia athari za miundo ya familia iliyodhoofika kwa utunzaji wa wazee, akisema, “Wizara itashirikiana na Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuhakikisha nyumba za malezi kwa wazee zinadhibitiwa vyema, kama vile nyumba za watoto zinavyodhibitiwa.”

Wakati serikali haiendelezi kikamilifu malezi ya kitaasisi, Gidudu alikiri kuwa elimu ya lazima kwa watoto na uhamiaji wa haraka mijini umefanya kuwa vigumu kwa familia kuhudumia jamaa wazee katika maeneo ya vijijini.

“Taarifa za ufuatiliaji za Wizara zinaonyesha kuwa nyumba nyingi za sekta binafsi zimeanzishwa kushughulikia huduma za wazee kutokana na ratiba nyingi za kazi za walezi na gharama kubwa za matunzo ya nyumbani,” Gidudu aliongeza.

All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment