Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa
Mkuu wa tume ya haki za binadamu ya umoja wa mataifa, Filippo Grandi, ameelezea kusikitishwa na hali inayoendelea kushuhudiwa nchini Sudan kutokana na vita ambavyo amesema vimesababisha raia wa nchi hiyo kukimbilia katika nchi za kigeni.

Tangu kuanza kwa vita Aprili mwaka jana, zaidi ya raia wa Sudan milioni 10 wamekimbia makazi yao, milioni mbili kati yao wakilazimika kukimbia nchi hiyo.
Katika mahojiano na shirika la habari la AFP kuelekea mkutano mkuu wa baraza kuu la umoja wa mataifa juma hili, Grandi amesema kutokana na mitandao mingi ya ulanguzi wa binadamu, raia wengi wa Sudan wanaweza na hata baadhi yao tayrai wanajaribu kuchukua boti zinazoelekea nchini Italia na nchi za ulaya.

Kulingana na Grandi, hata kabla ya vita vya Gaza, vita vya Sudan vilikuwa vimetengwa licha ya atahri zake, huku akikosoa jamii ya kimataifa kwa kupuuza mizozo barani Afrika, ikiwemo ya nchini DRC na eneo la Sahel.
Grandi aidha ameibua maswali kuhusu mustakabali wa Sudan hata kama amani itapatikana, akionya kuwa tayari raia wa Sudan wa tabaka la kati waliokuwa wanishikilia nchi pamoja wameharibiwa kabisa.
Vita vya Sudan vinavyohusisha jeshi linaloongozwa na Abdel Fattah al- Burhan na wapiganaji wa kundi la RSF chini ya uongozi wa Mohamed Hamdan Dagalo, vimesababisha vifo vya maelfu ya watu huku mamilioni ya wengine wakikumbwa na ukosefu wa usalama wa chakula.
All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.