Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa
Mkuu wa operesheni za umoja wa Mataifa za kulinda amani, Jean-Pierre Lacroix, jana jioni aliwasili nchini DRC, ambako hivi leo ataanza ziara ya siku tano kwenye taifa hilo.

Baadae hivi leo, Lacroix, anatarajiwa kukutana na rais Felix Tshisekedi, waziri mkuu Judith Suminwa pamoja na mawaziri wengine waliochaguliwa hivi karibuni kwenye serikali.
Katika ziara yake, mjumbe huyo wa katibu mkuu atajadiliana na viongozi wa nchi hiyo, kuhusu usalama na hali ya kibinadamu mashariki mwa nchi, wakati huu vikosi vya kulinda amani MONUSCO vikiendelea kuondoka.

Aidha, atajadiliana kuhusu mchakato wa mazungumzo ya amani yanayo ratibiwa na Angola ambayo yanaungwa mkono na umoja wa Mataifa pamoja na ushirikiano kati ya vikosi vya MONUSCO na vile SAMIDRC katika kutoa ulinzi wa raia huko Kivu Kaskazini na Ituri.
Lacroix pia atatembelea eneo la mashariki mwa nchi ambako atakutana na wahanga wa machafuko yanayoendelea.
All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.