Radio Fortune Africa-Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa
Mkutano wa ushirikiano kati ya mataifa ya Afrika na China, unaanza leo jijini Beijing baada ya kuwasili kwa viongozi mbalimbali wa Afrika.
Cheza – 00:56
Kwenye mkutano huo, ushirikiano kwenye masuala ya uchumi hasa maendeleo ya miundo mbinu ndio ajenda kubwa inayowaleta pamoja viongozi wa mataifa ya Afrika na nchi ya China.
Waziri wa Mambo ya nje wa China, Wang Yi amesema makubaliano yatakayoafikiwa kwenye mkutano huo, yanalenga kuimarisha zaidi uhusiano wa Afrika na China, lakini pia kuwawezesha watu kupata maendeleo.

China inatarajiwa kutangaza ahadi ya uwekezaji mkubwa kwa ujenzi wa miundombinu barani Afrika kwa kutoa mikopo ya fedha kwa mataifa mbalimbali , na kutoa mchango wa kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi kwa mataifa ya Afrika.
Wakuu wa mataifa ya Afrika pia kupitia mkutano huu, wanatarajiwa kufungua milango zaidi kwa wawekezaji wa China kwenye nchi zao, kuwekeza kwenye sekta mbambali kama madini na kilimo.
Masuala ya uongozi, siasa na usalama, pia yatajadiliwa kwenye mkutano huo unaoanza leo hadi siku ya Ijumaa.
All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.