
Chelsea wanataka kumsajili mshambuliaji wa Brentford na England Ivan Toney, 28. The Blues hata hivyo hawataweza kufikia mshahara unaopendekezwa na klabu ya Al-Ahli ya Saudi Arabia. (Sky Sports)
Toney anaweza kulipwa hadi £400,000 kwa wiki akiamua kujiunga na klabu hiyo ya Saudi Pro League. (Mail)
Newcastle na Manchester United wanatazamia kumnunua mshambuliaji wa England Dominic Calvert-Lewin, 27, ambaye mkataba wake unamalizika Everton msimu ujao. (Football Insider)

Liverpool wanawania kukamilisha usajili wa mshambulizi wa Juventus na Italia Federico Chiesa, 26, kabla ya dirisha la uhamisho kufungwa Ijumaa. (Athletic – usajili unahitajika)
Kiungo wa kati wa Lyon na Ubelgiji Orel Mangala, 26, anatarajiwa kufanyiwa vipimo vya afya na Everton kwa nia ya kujiunga na klabu hiyo kwa mkopo kabla ya tarehe ya mwisho ya uhamisho wa wachezaji. (Sky Sports)
Leicester wanakaribia kufikia mafanikio katika ombi lao la pauni milioni 19.5 kumnunua kiungo wa kati wa Genk na Morocco Bilal El Khannouss, 20. (Daily Telegraph – usajili unahitajika), kutoka nje.
Nottingham Forest inamnyatia mshambuliaji wa Ajax na Uholanzi Brian Brobbey, 22, na huenda wakamsajiliwa kabla ya dirisha la uhamisho kufungwa. (Mirror)Soma pia:
All Rights Reserved © Cantona Group PLC
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.