Netanyahu aenda Marekani kuujadili mpango wa nyuklia wa Iran

Radio Fortune Africa -Ukweli na Burudani

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Vocalize Pre-Player Loader

Na : Cantona Joseph|RFA

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amekwenda marekani kuzungumza na Rais Donald Trump kuhusu mpango wa nyuklia wa IranPicha: Jim Watson/AFP

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu anaelekea Marekani hii leo ambapo watajadiliana na Rais Donald Trump kuhusu mazungumzo ya nyuklia ya Iran.

Marekani Palm Beach 2025/Donald Trump na Benjamin Netanyahu katika mkutano wa habari.

Israel inashinikiza makubaliano hayo yajumuishe Iran kusitisha urutubishwaji wa aina yoyote wa madini ya urani, kupunguza mipango yake ya makombora na kuacha kuwasaidia makundi ya wanamgambo kama ya Hamas na Hezbollah.

Lakini Iran inayapinga masharti hayo na kusema itakubaliana tu na kiwango fulani cha ukomo kwenye mpango wa nyuklia ili badala yake iondolewe vikwazo vya kiuchumi.

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje wa Iran Esmail Baqaei mapema leo ameilaumu Israel kwa kupinga kila mchakato wa kidiplomasia unaolenga kuleta amani ya kikanda.

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment