Radio Fortune Africa -Ukweli na Burudani
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Na : Cantona Joseph|RFA

Baraza la mawaziri la Zimbabwe limeidhinisha rasimu ya sheria ambayo itamruhusu Rais Emmerson Mnangagwa, 83, kuongeza muda wake wa kukaa madarakani hadi angalau 2030.
Marais wangechaguliwa na wabunge badala ya kura ya moja kwa moja na wanaweza kuhudumu kwa muda usiozidi mihula miwili ya miaka saba, badala ya mihula ya sasa ya miaka mitano, chini ya mapendekezo hayo.
Waziri wa Sheria Ziyambi Ziyambi alisema mashauriano ya umma yatafanyika kabla ya mswada huo kuelekea bungeni kwa mjadala, ambapo mabunge yote mawili yanaongozwa na chama tawala cha Zanu-PF.
Changamoto za kisheria zinawezekana kwani wataalam wa kikatiba wanahoji kuwa kura ya maoni inahitajika ikiwa ukomo wa muda utabadilishwa – na pia wanasema kuwa marekebisho hayo hayawezi kumnufaisha rais aliyepo.
Mnangagwa, ambaye aliingia madarakani kwa mara ya kwanza mwaka 2017 baada ya mapinduzi ya kijeshi yaliyomuondoa madarakani kiongozi wa muda mrefu Robert Mugabe, alishinda uchaguzi wa urais mwaka uliofuata na muhula wa pili 2023 – ingawa matokeo yalipingwa.
Anajulikana kama “mamba” kwa sababu ya ujanja wake wa kisiasa, muhula wake wa mwisho wa miaka mitano unatarajiwa kumalizika mnamo 2028.
Katika kura ya maoni iliyofanyika miaka 13 iliyopita, Wazimbabwe waliipigia kura kwa wingi katiba mpya ambayo ilianzisha ukomo wa mihula ya urais wakati ung’ang’anizi wa Mugabe madarakani ulionekana kuimarika – aliiongoza nchi hiyo tangu uhuru mwaka 1980.
Britney Spears auza haki za muziki wake

Mwimbaji nyota wa muziki aina ya Pop Britney Spears ameuza haki za orodha yake yote ya muziki, BBC imebaini.
Spears, 44, inasemekana aliuza haki hizo kwa mchapishaji huru wa muziki wa Primary Wave tarehe 30 Desemba kwa karibu $200m (£146m).
Mwimbaji huyo – ambaye uhifadhi wake wa muda mrefu uliamuru maisha yake ya kibinafsi na kitaaluma – anajulikana kwa vibao …Baby One More Time, Oops!… I Did It Again, Toxic na Gimme More.
Primary Wave haikujibu mara moja maombi ya BBC ya kutoa maoni.
Wawakilishi wa Spears walikataa kutoa maoni.
Mnamo Januari 2024, mwimbaji huyo alisema “hatarudi tena kwenye tasnia ya muziki”.
Wimbo wake wa mwisho aliimba pamoja na mwanamuziki Elton John mnamo 2022.
Tunachojua kufikia sasa kuhusu shambulio la Shule nchini Canada
RCMP, jeshi la polisi la shirikisho la Canada sawa na FBI ya Marekani, wamemaliza mkutano wao na wanahabari ambapo afisa mkuu wa polisi Chief Supt Floyd alizungumza, lakini alitoa majibu machache kuhusu kile kilichotokea. Tunachojua ni kwamba:
- Takriban wanafunzi 100 na wafanyikazi walihamishwa kutoka shuleni baada ya maafisa kufika, wakiitikia wito wa mtu aliyefyatua risasi.
- Polisi wanaamini kuwa wamemtambua mshambuliaji, lakini hawajatoa jina lake hadharani
- Chanzo cha shambulio hilo hakijajulikana kwa sasa, alisema, na kuongeza: “Nadhani tutajitahidi kubaini ‘kwanini’, lakini tutajaribu tuwezavyo kubaini ni nini kilifanyika”
- Alikataa kusema ni watoto wangapi waliathiriwa na tukio la ufyatuaji risasi katika shule hiyo na katika nyumba jirani, lakini akaongeza kuwa wachunguzi bado hawako tayari kushirikisha uhusiano wowote.
Tutakuletea maelezo zaidi mara tu tutakapoyapata.
Baba alimpiga risasi binti yake baada ya ‘kubishana kuhusu Donald Trump’

Mwanamke wa Uingereza ambaye aliuawa kwa kupigwa risasi na babake alipokuwa akizuru nyumbani kwake huko Texas alikuwa amebishana naye kuhusu Rais wa Marekani Donald Trump mapema siku hiyo, uchunguzi umeelezwa.
Lucy Harrison, kutoka Warrington huko Cheshire, alipigwa risasi kifuani tarehe 10 Januari 2025 huko Prosper, karibu na Dallas.
Polisi katika mji huo walichunguza kifo cha kijana huyo mwenye umri wa miaka 23 kama mauaji ya bila kukusudia lakini hakuna kesi ya jinai iliyoletwa dhidi ya Kris Harrison baada ya mahakama kuu katika kaunti ya Collin kukataa kumfungulia mashtaka.
Uchunguzi wa kifo cha Lucy Harrison ulianzishwa mapema katika Mahakama ya Cheshire Coroner, ambapo mpenzi wake Sam Littler alielezea “mabishano makubwa” kuhusu Trump, ambaye alikuwa akijiandaa kuapishwa kwa muhula wake wa pili
Watu tisa wauawa kwa kupigwa risasi, wakiwemo saba shuleni Canada – Polisi

Takriban watu tisa wameuawa kwa kupigwa risasi magharibi mwa Canada, kulingana na maafisa wa polisi wa Royal Canadian Mounted Police (RCMP).
Waathiriwa sita waligunduliwa katika Shule ya Sekondari ya Tumbler Ridge kaskazini-mashariki mwa British Columbia, RCMP inasema.
Mmoja wa saba alifariki akiwa njiani kupelekwa hospitali.
Wengine wawili walikutwa wamekufa katika eneo lingine, ambalo polisi wanaamini kuwa lina uhusiano na tukio hilo. Takriban watu wengine 25 wamejeruhiwa.
Mtu anayeaminika kuwa mpiga risasi pia alipatikana amekufa na kile kilichoonekana kuwa ni jeraha la kujidhuru, polisi wanasema.
Wabunge wa Marekani wamtaka kakake mfalme wa Uingereza kutoa ushahidi juu ya faili za Epstein

Andrew Mountbatten-Windsor Kakake mfalme wa Uingereza anakabiliwa na shinikizo kubwa kutoka kwa maafisa wa Marekani na familia ya mshtaki wake mashuhuri Virginia Giuffre kutoa ushahidi nchini humo juu ya uhusiano wake na mfadhili wa wanaonyanyasa watoto kingono Jeffrey Epstein.
Mbunge wa Democrat Ro Khanna alisema Familia ya Kifalme “haikuwa wazi”, wakati mbunge Teresa Leger Fernandez, pia Mdemokrat, alisema “Mfalme anapaswa kumuelekeza kaka yake” kwenda Marekani kujibu maswali.
Mapema Jumanne, Mfalme Charles III alisema Familia yake ilikuwa “tayari kusaidia” polisi katika maswali yao.
Andrew amerudia kukana kosa lolote na kufikia suluhu nje ya mahakama na Giuffre mnamo 2022.
Trump atangaza uwezekano wa kutuma meli nyengine ya kubeba ndege za kivita katika Ghuba ya Uajemi

Rais wa Marekani ametangaza uwezekano wa kutuma chombo kingine cha kubeba ndege pamoja na meli yake kwenye Ghuba ya Uajemi na wakati huo huo akaeleza matumaini yake kuhusu manufaa ya mazungumzo hayo na Iran.
Axios aliandika Jumanne, Februari 10, kwamba Donald Trump alisema: “Tuna meli ya wanamaji inayoelekea huko na nyingine inaweza kutumwa.”
Hii inamaanisha kuwa pamoja na shehena ya ndege ya Abraham Lincoln na meli inayoandamana nayo, ambayo ni pamoja na waangamizi kadhaa na makombora ya Tomahawk, kundi lingine linatumwa kwenye Ghuba ya Uajemi.
Rais wa Marekani aliiambia Axios kwamba kwa kuwa viongozi wa Iran hawakukataza mashambulizi ya kijeshi katika mazungumzo kabla ya vita vya siku 12, wakati huu itakuwa “tofauti sana.”
Bw. Trump, akiwa na matumaini kuhusu njia ya diplomasia, alisema Iran “inataka sana” makubaliano na imeingia kwenye mazungumzo kwa umakini zaidi wakati huu kwa sababu ya tishio la kijeshi.
Duru ya kwanza ya mazungumzo ya nyuklia kati ya Tehran na Washington ilifanyika Ijumaa iliyopita huko Muscat, mji mkuu wa Oman, na pande hizo mbili zilikubaliana kuendelea na mazungumzo hayo.
All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2026
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.