Radio Fortune Africa -Ukweli na Burudani
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Na : Cantona Joseph|RFA

Makamu Mwenyekiti wa chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), John Heche, pamoja na viongozi wengine wa chama hicho wameachiwa kwa dhamana, hatua ambayo imethibitishwa rasmi na CHADEMA.
Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na chama hicho, Heche alikuwa akikabiliwa na matatizo ya kiafya alipokuwa chini ya ulinzi wa polisi, na leo polisi walimpeleka hospitalini kwa matibabu kabla ya kumuachia.
Heche alikamatwa zaidi ya wiki tatu zilizopita bila kufikishwa mahakamani, na hata familia yake haikujua alipo.
Baadaye, alipelekwa kituo cha polisi na kusomewa mashtaka ya ugaidi
Miongoni mwa viongozi wengine wa CHADEMA walioachiwa kwa dhamana ni Naibu Katibu Mkuu Bara, Amani Golugwa, aliyekuwa Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, na aliyekuwa Meya wa Manispaa ya Ubungo, Boniface Jacob.
Viongozi hao walikamatwa kwa tuhuma za kuchochea maandamano yaliyodaiwa kulenga kuzuia kufanyika kwa uchaguzi mkuu.
Wakati hayo yakijiri, Mahakama leo imeahirisha kusikiliza kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA Tundu Lissu kwa kile kilichotajwa kuwa ni sababu za kiusalama.
Kesi hiyo imepangwa kuendelea tena tarehe 12 mwezi Novemba.
All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.