Radio Fortune Africa -Ukweli na Burudani
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Na : Cantona Joseph|RFA

Rais wa Syria Ahmed al-Sharaa amewasili Marekani (Jumamosi usiku) kwa ziara rasmi ya kihistoria, kwa mujibu wa shirika rasmi la habari la Syria, siku moja baada ya Washington kuliondoa jina lake kwenye orodha yake ya magaidi.
Al-Sharaa anatarajiwa kukutana na Rais wa Marekani Donald Trump katika Ikulu ya White House siku ya Jumatatu, ikiwa ni ziara ya kwanza ya aina hiyo kufanywa na rais wa Syria tangu nchi hiyo ilipopata uhuru wake mwaka 1946.
Al-Sharaa alikutana kwa mara ya kwanza na Trump katika mji mkuu wa Saudia, Riyadh, wakati wa ziara ya kikanda ya rais huyo wa Marekani mwezi Mei.
Mjumbe wa Marekani nchini Syria, Tom Barrack, mapema mwezi huu alisema kwamba Al-Sharaa itatia saini makubaliano ya kujiunga na muungano wa kimataifa unaoongozwa na Marekani dhidi ya kundi la Islamic State.
Chanzo cha kidiplomasia nchini Syria kiliiambia shirika la habari la AFP kwamba Marekani inapanga kuanzisha kituo cha kijeshi karibu na mji wa Damascus “kuratibu misaada ya kibinadamu na kufuatilia hali kati ya Syria na Israel.”
Vyanzo vinavyofahamu suala hilo vililithibitishia shirika la habari la Reuters hapo awali kwamba Washington inajiandaa kupeleka wanajeshi katika kambi ya wanahewa mjini Damascus ili kusaidia utekelezaji wa makubaliano ya kiusalama kati ya Syria na Israel ambayo yaliyosimamiwa na Marekani.
Trump na al-Sharaa pia wamepangwa kujadili mazungumzo ya moja kwa moja kati ya mamlaka ya Syria na Israel.
All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.